BI REHEMA AANZA MATIBABU KATIKA HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI
Bi Rehema Juma Kishena kama anavyoonekana pichani anayesumbuliwa na uvimbe kwa takribani miaka 17.Picha na Vero Ignatus Blog.
Na.Vero Ignatus Arusha.
Hatimae Rehema Juma Kishena (40) aliyekuwa anaomba msaada wa matibabu kutokana na uvimbe unaomsumbua kwa miaka 17 amefanikiwa kwenda hospitalini kwaajili ya matibabu
Bi.Rehema kupitia msaada wa wasamaria wema walioweza kumsaidia kwa kiwango cha fedha kidogo tarehe 22/8/2017 alifanikiwa kwenda hospitali ya KCMC akampatia rufaa kuelekea Muhimbili leo tarehe 28/8/2017
Akizungumza na mwandishi wa blog hii dada wa Mgonjwa Aziza Bakari Muyai amesema kuwa tayari siku ya leo wamefika hospitali ya Muhimbili wanatarajia majibu kutoka kwa madaktari watakaomuhudumia mgojwa ili waelewe hatua itakayofuata.
Aidha Bi Aziza amewashukuru wale wote waliomsaidia hadi mdogo wake Kuanza matibabu ,amewaomba wasichoke kwani hali ya mgonjwa bado haijatengamaa.
Bi Rehema Juma Kishena (40) amelazwa Katika hospitali ya Muhimbili Jengo la Sewa Haji, Wodi namba 24 Kitanda namba 16
Uongozi wa Blog hii unatoa shukrani kwa Wale wote waliosoma habari kuhusiana na tatizo linalomsumbua Rehema kupekekea kuomba msaada wa matibabu, tunawashukuru wale wote waliojitoa kwa hali na mali ili kuhakikisha kuwa Bi Rehema anapatiwa matibabu Mungu awazidishie kila mlipotoa.
Bi Rehema Kushoto akiwa na dada yake Bi. Aziza Bakari wakiwa nje ya Hospitali ya Kcmc hapo Juzi.Picha kwa hisani ya Bi Aziza Bakari.
Bi Rehema Juma akiwa ameshapatiwa Kitanda Katika Hospitali ya Muhimbili Leo wodi mamba 24 kitanda namba 16. Picha kwa hisani ya bi Aziza Bakari
Na.Vero Ignatus Arusha.
Hatimae Rehema Juma Kishena (40) aliyekuwa anaomba msaada wa matibabu kutokana na uvimbe unaomsumbua kwa miaka 17 amefanikiwa kwenda hospitalini kwaajili ya matibabu
Bi.Rehema kupitia msaada wa wasamaria wema walioweza kumsaidia kwa kiwango cha fedha kidogo tarehe 22/8/2017 alifanikiwa kwenda hospitali ya KCMC akampatia rufaa kuelekea Muhimbili leo tarehe 28/8/2017
Akizungumza na mwandishi wa blog hii dada wa Mgonjwa Aziza Bakari Muyai amesema kuwa tayari siku ya leo wamefika hospitali ya Muhimbili wanatarajia majibu kutoka kwa madaktari watakaomuhudumia mgojwa ili waelewe hatua itakayofuata.
Aidha Bi Aziza amewashukuru wale wote waliomsaidia hadi mdogo wake Kuanza matibabu ,amewaomba wasichoke kwani hali ya mgonjwa bado haijatengamaa.
Bi Rehema Juma Kishena (40) amelazwa Katika hospitali ya Muhimbili Jengo la Sewa Haji, Wodi namba 24 Kitanda namba 16
Uongozi wa Blog hii unatoa shukrani kwa Wale wote waliosoma habari kuhusiana na tatizo linalomsumbua Rehema kupekekea kuomba msaada wa matibabu, tunawashukuru wale wote waliojitoa kwa hali na mali ili kuhakikisha kuwa Bi Rehema anapatiwa matibabu Mungu awazidishie kila mlipotoa.
| Ameomba kwa yeyote aliyepo tayari kumsaidia atumie mawasiliano kwa namba0653179373 |

No comments