RUFAA YA LEMA YAPIGWA KALENDA.
Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema( pichani)
Na. Vero Ignatus-Arusha
Rufaa
namba 49/2017 ya mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema imesogezwa mbele
kwa ajili ya kutolewa maamuzi mara baada ya upande wa Jamhuri kuiomba
mahakama kuu jijini Arusha kuweza kujibizana kwa maandishi juu ya rufaa
hiyo ambapo pia jamhuri imesema hawaku pewa nakala ya rufaa hiyo.
Rufaa
hiyo imekuja Mara baada ya lema kufunguliwa kesi ya inayodaiwa kuwa ni
ya uchochezi katika mitandao ya kijamii kusambaza kipande cha video
kinacho hamasisha maandamo mnamo tarehe 1/9/2016 kuweza kumpinga rais
Dkt John pombe magufuli.
Wakili Shedraki Mfinanga anaemtetea mbunge Godbless lema amesema kuwa rufaa hiyo kushindwa kutolewa maamuzi na jaji Dkt Modest Opiyo mahakama
kuu ya Arusha ,wameomba wafanye majadiliano kwa njia ya maandishi kwa upande wa jamhuri na upande wa Lema ili waweze kufikia muafaka.
Kwa
mujibu wa Jaji Dkt. Modest Opiyo uamuzi wa rufaa hiyo unatarajiwa
kutolewa tarehe 27/09/2017 Mara baada ya kusikiza hoja za pande zote.
| |||

No comments