VIONGOZI WALIOPEWA DHAMANA YA KUONGOZA NCHI WAMETAKIWA KUACHA UBINAFSI ULIOKITHIRI ,WASIWE WASANII NA WASIMDANGANYE MUNGU


Askofu mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri nchini Tanzania (KKKT)Dkt. Fredrick Shoo akiwa katika ibada katika usharika wa Kiborloni uliopo Moshi mkoani Kilimanjaro.

Askofu  mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri nchini Tanzania  (KKKT)Fredrick  Onael  Shoo  amewataka viongozi ambao wanadhamana ya kuongoza nchi  waondokane na ubinafsi uliokithiri kwa kuwadidimiza wengine ,wasiwe waigizaji ,waepuke kuwa mateka wa kupokea rushwa kwani wanaweza kuwadanganya wanadamu ila hawawezi kumficha Mugu.
 Ameyasema hayo hivi karibuni mkoani Kilimanjaro katika ibada ya kumuaga aliyewahi kuwa mbunge wa Moshi mjini marehemu Dkt. Philemon Ndesamburo ambapo alisema Mungu amewapa nafasi hivyo waitumie  vyema kwa kutumikia nafasi zao waachane na maneno yasiyokuwa na faida.

“Wacheni maneno maneno watendeeni wananchi mema,Mungu akikupa nafasi itumie vyema,viongozi msichoke kutenda mema  fahamuni kuwa uongozi ni dhamana mtakwenda kuulizwa mlifanyaje siku ya mwisho”.alisema askofu huyo.

Aidha amesema kuwa maisha ya kila mwanadamu yana mpaka ambao hauwezi kuuvuka kamwe kwani ikifika wakati wa kuondoka utaondoka tu hakuna kipingamizi ila ni vyema kila mtu akaandaa maisha yake  kwani ni siri kubwa aliyoiweka kwa mwanadamu.
Askofu Fredrick Shoo akiwa anaendesha ibada usharika wa Kiborloni Moshi mkoani Kilimanjaro

Askofu Dkt Fredrick Shoo  aliwataka viongozi wa vyama vya siasa na Serikali, kusimamia katika kutenda haki na kusaidia makundi ya kijamii, kwani wapo wanaoumizwa kwa kukosa haki zao kutokana na umasikini pia aliwataka waumini na Watanzania kujifunza na kusimamia katika kutetea haki za wanyonge na makundi mengine ya kijamii.

 “Ndesamburo nimemfahamu muda mrefu, alikuwa mtu makini, alisimamia haki na kutetea wanyonge... kazi aliyoiacha itaendelea kusimama kama maandiko matakatifu yanavyoelekeza, alipigania demokrasia, tusiogope katika kusema kweli,” alisema.
 
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Willium Lukuvi ambaye alihudhuria katika msiba huo alisisitiza kuwa serikali inathamini mchango wa Ndesamburo katika maendeleo ya taifa ambapo amesema kuwa Ndesamburo alikuwa kiunganishi bila kujali itikadi za vyama. 

Kwa upande wake Kiongozi wa Upinzani bungeni na mwenyekiti wa Chadema Taifa Freeman Mbowe alisema kuwa msiba huo ni pengo kubwa sana kwao amesema watakachoweza kukufanya ni kuenzi kazi za Ndesamburo kwa ni alikuwa mpenda haki na mtetezi wa wanyonge.
  
Alimuomba Waziri Lukuvi ambaye pia ni mbunge awasilishe kwa viongozi wa serikali kuwa wabunge wa chadema siyo wakorofi wala hawana utaratibu wa kugoma bali ni pale tu baadhi ya viongozi wa serikali wanapotoa matamko na hawataki kusikiliza kauli za wengine hatutakaa kimya kwani utakuwa ni unafiki.

Mbali na Waziri Lukuvi, wengine walioshiriki maziko hayo ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro, Iddi Juma na Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe, mawaziri wakuu wastaafu, Edward Lowassa na Frederick Sumaye ambao pia ni wajumbe wa Kamati Kuu ya Chadema na viongozi wengine waandamizi wa chama hicho kutoka makao makuu na mikoa mbalimbali.

 Dkt.Philemon Ndesamburo alizikwa nyumbani kwake mtaa wa KDC Kata ya Kiboriloni Manispaa ya Moshi, baada ya kufariki ghafla Mei 31, mwaka huu. Alijisikia vibaya akiwa ofisini kwake na alifariki akiwa njiani kupelekwa hospitalini,


Jeneza lilobeba mwili wa mehemu Philemon Dkt Philemon Ndesamburo
 










 
 
Image result for gari lililobeba mwili wa ndesamburo

Image result for gari lililobeba mwili wa ndesamburo
Gari lililobeba mwili wa Dkt Philemon Ndesamburo likiingia katika eneo la kanisa la KKKT Usharika wa Kiborloni Moshi Kilimanjaro 
        
Image result for gari lililobeba mwili wa ndesamburo
Kaburi alimozikwa Dkt Philemon Ndesamburo











No comments