JAJI SEKELA:MAHAKAMA INATEGEMEA USHIRIKIANO MKUBWA KUTOKA KWA WADAU WENGINE ILI KUWEZESHA UKUAJI WA UCHUMI




Kaimu Jaji Mfawidhi Mahakama kuu Kanda ya Arusha akisoma hotuba siku ya Maadhimisho ya siku ya  Sheria nchini.Picha na Vero Ignatus Blog
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Mashaka Gambo akizungumza katika viwanja vya mahakama kuu katika siku ya sheria nchini,ambapo amewaambia Majaji,mawakili,Mahakimu pamoja na mawakili,kuwa kazi yao ni ngumu inahitajika wawe na hofu ya Mungu,Picha na Vero Ignatus Blog.

Maheshimiwa Majaji wakiwa wanabadilishana mawili matatu kama wanavyoonekana katika picha na mstahiki meya wa Jiji la Arusha Calist Lazaro.Picha na Vero Ignatus Blog.
Wakili Magdalena Sylister akisalimiana na Mwandishi wa habari John Muhala katika maadhimisho ya siku ya sheria nchini .Picha na Vero Ignatus Blog.

Waheshimiwa majaji pamoja na mkuu wa mkoa wa Arusha wakiwa katika picha ya pamoja na mahakimu katika siku ya maadhimisho ya sheria nchini katika viwanja vya mahakama kuu kanda ya Arusha picha na Vero Ignatus Blog.




Aliyeko kulia ni Mhe,Jaji Salma Magimbi,Jaji wa mahakama kuu Kanda ya Arusha,akifuatiwa na aliyeko kulia kushoto kwake Kaimu Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu kanda ya Arusha Mhe,Sekela Cyril Moshi,kifuatiwa na Mkuu wa mkoa wa Arusha Misho Mashaka Gambo ,na wa kwanza kulia ni Mhe,Jaji Dk.Modesta Opiyo,Jaji wa mahakama kuu kanda ya Arusha ,wakiwa katika picha ya pamoja katika maadhimisho ya siku ya sheria nchini wakiwa na viongozi wa dini.
Baadhi ya Mahakimu na Mawakili wa Serikali na wale wa kujitegemea  wakiwa katika viwanja vya Mahakama kuu Kanda ya Arusha wakiwa katika maadhimisho ya siku ya sheria nchini.Picha na Vero Ignatus Blog.
Askari Polisi ,pamoja na na askari wa Jeshi la Magereza wakiwa pamoja katika Mahakama kuu Kanda ya Arusha katika maadhimisho ya  siku ya sheria nchini.Picha na Vero Ignatus Blog.
Wakili Magdalena Sylister akisalimiana na Mwandishi wa habari John Muhala katika maadhimisho ya siku ya sheria nchini .Picha na Vero Ignatus Blog.
Baadhi ya Mahakimu na Mawakili wa Serikali na wale wa kujitegemea  wakiwa katika viwanja vya Mahakama kuu Kanda ya Arusha wakiwa katika maadhimisho ya siku ya sheria nchini.Picha na Vero Ignatus Blog.

Waheshimiwa Mjaji wakiwa katika picha ya pamoja na Mahakkimu katika siku ya sheria nchini katika viwanja vya Mahakama kuu kanda ya Arusha .Picha na Vero Ignatus.

Mhe,Jaji Dk.Modesta Opiyo Jaji wa mahakama kuu Kanda ya Arusha akitoa neno la shukrani kwa wageni mbalimbali waliohudhuria katika siku ya sheria nchini.Picha na Vero Ignatus Blog.
Kikundi cha Burudani kikifanya yao katika maadhimisho ya siku ya sheria nchini katika viwanja vya Mahakama kuu kanda ya Arusha .Picha na Vero Ignatus Blog.



 
 Wanafunzi wa chuo kikuu Makumira kitivo cha sheria wakiwa katika picha ya pamoja na waheshimiwa Majaji ,mkuu wa mkoa wa Arusha ,katika siku ya sheria nchini .Picha na Vero Ignatus Blog.

Na Vero Ignatus. Blog

Mahakama kuu kanda ya Arusha imeungana na na mahakama nyingine kuadhimisha siku ya sheria nchini ambapo ni siku ya kuanza rasmi shughuli za mahakama,ikiwa na Maudhui yanayosomeka ‘Umuhimu wa utoaji haki kwa wakati kuwezesha ukuaji wa uchumi.


Akisoma hotuba Kaimu Jaji mfawidhi wa mahakama kuu kanda ya Arusha Jaji Sekela Cyril Moshi amesema kuwa katika kuadhimisha siku ya sheria 2017 amesema kuwa neono haki katika sheria hasa mahakama lina maana ya stahiki ambayo mtu anastahili kuipata kwa mujibu wa sheria ,taratibu na kanuni zilizowekwa katika upatikanaji wa kitu au jambo hilo.


Jaji Sekela amesema kuwa ili kuboresha na kufanikisha malengo ya kutoa haki kwa wakati ili kusaidia kukuza uchumi ,Mahakama inahitaji kuwezeshwa kwa rasilimali kama fedha za kutosha na pesa hizi zipatikane kwa wakati,upatikanaji wa rasilimali utasaidia mahakama kutimiza majukumu yake kwa wakati.


Ametoa rai kwa watu wote kuwa ,malengo haya ya kumaliza kesi kwa wakati ili kuwezesha ukuaji wa uchumi hayawezi kufanikishwa na mahakama peke yake,inategemea ushirikiano mkubwa kutoka kwa wadau wengine wakiwemo wadau,mawakili wa serikali na wakujitegemea,magereza na taasisi zingine za serikali zikiwemo Takukuru ,hivyo ameiomba jamii ishirikiane na kusaidiana ili kufikia malengo waliyojiwekea


“Vyombo vyenye mamlaka ya kutekeleza utoaji haki vitakua ni mahakama ya serikali ya Jamhuri ya muungano wa Mahakama ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,Mamlaka ya utoaji haki jamhuri ya muungano ipo mikononi mwa mahakama ya Tanzania na mahakama ya Zanzibar ,na kwahiyo hakuna chombo cha serikali wala cha bunge au Baraza la wawakilishi la Zanzibar kitakachokuwa na kauli ya mwisho katika utoaji haki”alisema Jaji Sekela.


Amesema kuwa ibara ya 107A(2)ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeweka misingi ya utoaji haki amabayo mahakama inapaswa kuizingatia katika kutekeleza majukumu yake ya kikatiba,kutenda haki ya mtu kijamii,au kiutamaduni,kutochelewesha haki bila sababu ya msingi,kutoa fidia ipasavyo kwa watu wanaoathirika kutokana na makosa ya watu wengine,na kwa mujibu wa sheria mahususi iliyotungwa na Bunge.


Aidha amesema kuwa kutenda haki pasipo kufungwa kupita kiasi na masharti ya kiufundi yanayoweza kukwamisha haki kutendeka,kukuzana kuendeleza usuluhishi baina ya wanaohusika katika migogoro,ambapo mahakama inawajibika kutenda haki bila kuchelewa “Haki iliyocheleweshwa ni sawa na haki iliyokosekana”


Kwa upande wa hotuba iliyosomwa na mwenyekiti wa chama cha mawakili Tanganyika kanda ya Kaskazini ,wameiomba jeshi la polisi kuwahudumia wananchi kwa weledi na haki wazingatie sheria,wasitumie nguvu kupita kiasi,na wakamilishe upelelezi mapema kabla ya kumkamata mtuhumiwa.


Wamewapongeza Takukuru kwa utendaji wao kwani wamefanikiwa katika ukamataji wa watuhumiwa baada ya upelelezi kukamilika,mawakili hao wamewataka Jeshi la magereza wasichoke kuwahudumia mahabusu kwa huruma haswa ikizingatiwa kwamba hao hawajahukumiwa bado,huku wakiwataka baraza la Ardhi na nyumba wilaya waboreshe utendaji wao.


No comments