FAO YAAHIDI KUSHIRIKIANA NA SERIKALI ILI KUHAKIKISHA WAKULIMA WANAZALISHA CHAKULA CHA KUTOSHA


Wakwanza kushoto ni Bi Mary Kimambo  kutoka kituo cha utafiti cha Seliani kitengo cha maharagwe,akifuatiwa na aliyepo kushoto kwake ni Mkurugenzi wa fedha wa shirika hilo Drollah Ssebagala .Picha na Vero Ignatus Blog.
Ikunda Materu kutoka Baraza la nafaka la Afrika Mashariki,
Baadhi ya wakulima walioshiriki katika maonyesho hayo yaliyofanyika kwa siku mbili katika kituo cha utafiti cha Selian.Picha na Vero Ignatus Blog.
 Baadhi ya wakulima wakipate elimu kwenye shamba darasa katika maonyesho hayo yaliyofanyika katika kituo cha utafiti cha Seliani.Picha na Vero Ignatus Blog.
 Baadhi ya wadau wa zana za kilimo walioshiriki maonyesho hayo kutoka kampuni ya Wade Rain.Picha na Vero Ignatus Blog.
Afisa Maendeleo  Biashara kutoka Asasi isiyo ya kiserikali (PASS) Ayubu Mbezi (aliyevaa tisheti ya njano pichani)akitoa elimu kwa mkulima namna ambayo mkulima anaweza kuunganishwa na Taasisi hiyo kupata mkopo benki na kuwaonngezea dhamana aliyepo kulia kwake ni Peter Msechu mfanyakazi katika Taasisi hiyo.PASS inajishughulisha kusaidia sekta ya kilimo,iliyoanzishwa mwaka 2000 ili kuchbochea uwezeshaji na kukuza kilimo cha biashara na sekta zinazohusika.Picha na Vero Ignatus Blog.


 Mkufunzi Happy Martin  kutoka Taasisi isiyo ya kiserikalia (ECHO)dawa i akitoa elimu kwa wakulima namna ya kuhifadhi mbegu katika mazingizra maziri bila kuziweka dawa Mbegu bora zinatzoweza kama mbolea,mbegu.Picha na Vero Ignatus Blog.

Na.Vero Ignatus .Arusha


SHIRIKA la chakula Ulimwenguni, FAO, limeahidi  kuendelea kushirikiana
 na serikali katika kuhakikisha wakulima wanazalisha chakula cha kutosheleza na hivyo kuondoa tatizo la uhaba wa chakula kwa baadhi ya maeneo hapa nchini.


Mwakilishi wa FAO ,Fred Caferody,ameyasema hayo alipokuwa akitoa salamu kwenye siku ya wakulima wa mazao mchanganyiko ya chakula na biashara kutoka mikoa mbalimbali nchini yaliyofanyika kwenye viwanja wa Taasisi ya utafiti wa mazao, Seliani jijini Arusha.

Kwa upande wake Muwakilishi wa Baraza la nafaka la Afrika mashariki, (EAGC),hapa nchini Ikunda Materu alimesema litaendelea kushirikiana na vituo vya utafiti wa mazao ya kilimo kwa nchi za afrika mashariki  katika kutafuta masoko ya nje wakulima nchini.

Amesema FAO, imekuwepo hapa nchini kwa miaka 40 imekuwa ikiandaa sera na programu mbalimbali za kilimo na chakula ili kuwezesha wakulima kuzalisha chakula kinachotosheleza mahitaji kwa kushirikiana na serikali na swala la kilimo na chakula ni sehemu ya jukumu lake kuhakikisha hakuna upungufu wa chakula nchini.


Mkurugenzi wa fedha wa shirika hilo Drollah Ssebagala, amesema baraza la nafaka  litakuwa likiwapatia wakulima taarifa za masoko  kwenye nchi za Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Zambia DRC congo, Malawi na Zambia Sudani na Ethiopia


Kwa upande wake mkurugenzi mkuu wa utafiti wa mazao nchini kutoka wizara ya Kilimo na Mifugo, Dakta Jackson Nkuba, amesema upo ugonjwa wa Manjano unaoshambulia mahindi  na hilo ni tatizo kubwa hivi sasa serikali kupitia wizara ya kilimo imeweka nguvu kubwa ili kuudhibiti ugonjwa huo.

 Amesema kuwa ugonjwa huo ni tatizo kwa kuwa unashambulia mahindi yakiwa shambani na kunyauka hivyo mkulima anapata hasara .


Amesema kuwa hayo ni maonyesho ya nne ya mnyororo wa mazao ya kilimo kufanyika nchini ni maonyesho muhimu sana na yatapanuliwa katika kanda zingine nchini lengo ni kuwezesha wakulima kupata teknolojia ya kilimo cha biashara kutoka kilimo cha kujikimu .


Hivyo akayataka makampuni ya uzalishaji  wa mbegu bora kutoka kwenye taasisi za utafiti wa mbegu ambayo yataongezeka ili kuwafikia wakulima ili kuwafikia wakulima waweze kuzalisha mazao bora na kulima kilimo cha kibiashara.


Akifungua maonyesho hayo Katibu tawala wa mkoa wa Arusha, Richard Kwitega, amesema mpango wan chi katika kilimo ni kuendelea kushirikiana na  baraza la Nafaka la nchi za afrika mashariki,shirika la kilimo na chakula ulimwengini, FAO na wadau wengine

Amewataka watafiti wa mbegu kuhakikisha matokeo ya uutafiti wanazofanya yanawafikia wakulima ili kuweza klkuleta tija vinginecvyo yasiopowafikia walengwa hayawezi kuleta tija kwenye kilimo.


Amezitaka taasisi zingine binafsi kuongeza ushirikiano na serikali ili kuharakisha maendeleo na upatikanaji wa mbegu bora za mazao aina mbalimbali za mazao.


Amesema uzalishaji mdogo wa mazao unachangiwa na  kilimo kisichozingatia utaalamu ,ukosefu wa masoko mazao kushambiliwa na magonjwa ucheleweshwaji wa pembejeo  kutokuwepo kwa vikundi vya wakulima miundo mbinu hafifu  ya kuhifadhia mazao na kuendelea na kilimo cha kizamani.


Hivyo akatoa wito kwa wataalamu wa kilimo kuanzisha mashamba darasa kila eneo ili wakulima waweze kupata elimu na kubadilisha mbinu za kilimo kutoka cha kujikimu na kuwa cha kibiashara.


Akawataka viongozi wa vijiji kihakikisha kila kaya inatenga hekari moja yitakayotokana na kilimo cha mazao yanayotokana na mbegu bora zilizofanyiwa utafiti na hivyo kuharakisha mabadiliko .

No comments