WAZIRI NCHEMBA: MADEREVA WANAOACHA MAWE BARABARANI BAADA YA MATENGENEZO WACHUKULIWE HATUA KALI


Image result for waziri wa mambo ya ndani mwigulu nchemba
 Na Vero Ignatus.Singida.

Waziri wa mambo ya ndani Mwigulu Lameck Nchemba ameliagiza jeshila polisi kitengo cha usalama barabarani kuwachukulia hatua kali za kisheria  madereva ambao magari yao yanaharibika njiani 
wanaacha mawe makubwa  baada ya matengenezo ya magari hayo

 "Nawaagiza jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani chukueni alama na namba za magari yao haijalishi watakuwa wamevuka mikoa mingapi warudisheni waje wayaondoe mawe yao waliyoyaacha barabarani"alisema waziri.


Amesema leo katika ziara ya Rais Dkt.Magufuli mkoani Singida alipopewa nafasi ya kusalimia wananchi ambapo amesema kuwa kuwa jukumu la utunzaji wa barabara ni la kila mtu na siyo serikali peke yake hivyo ni vyema wananchi wakaelewa kuwa utengenezaji wa barabara umetumia kiasi kikubwa cha fedha. 
"wakati utengenezaji wa barabara unapoeendelea kila mtu anatamani iishe mapema ili itumike ,lakini wanasahau kuwa wanahitajika kuitunza ,kila mtu atunze barabara kwa maslahi ya Taifa letu"alisisitiza waziri.

Aidha amewataka madiwani wote kuwasaidia na kuwaelimusha jamii ya wafugaji namna ya kutumia vivuko vya wanyama vilipo na wavitumie ipasavyo ili wanyama wasiaharibu barabara.

"Tumuunge rais mkono katika juhudi zake ananzozifanya za kuleta maendeleo katika nchi hii"alisisitiza.

No comments