ALL STARS VETERAN KUFANYA BONANZA LA KUWAKUMBUKA WENZAO WALIOPOTEZA MAISHA SAME KILIMANJARO

Kamati maalum ya Maveterani wa timu ya soka ya Arusha All Star ya Jjijini Arusha wakijadili mambo muhimu kwaajili ya kuwaenzi Veterans waliopata ajali  mwaka 1990.picha na Vero Ignatus Blog
Denis Zakaria Mkurugenzi wa benchi la ufundi katika kikosi cha All Star akitoa ufafanuzi kuhusu bonanza maalum kuhusu kuadhimisha siku ya Veteran waliopata ajali wilayani Same  mkoani Kilimanjaro.Picha na Vero Ignatus Blog
Pichani ni Azizi Nyoni Kocha wa All Stars Veteran akizungumza kuhusiana na bonanza hilo .Picha na Vero ignatus Blog.

 
Kamati ikiendelea na kikao wakijadili mambo muhimu kwaajili ya kuwaenzi Veterans waliopata ajali  mwaka 1990.picha na Vero Ignatus Blog

 Na.Vero Ignatus Arusha
 
Katika kuwa kumbuka wanasoka waliopoteza maisha katika ajali wilayani same mnamo mwaka 1990 timu ya soka ya veteran Arusha all stars wameandaa bonanza maalumu kwa ajili kuwaenzi baadhi ya wachezaji waliopoteza maisha katika ajali hiyo mkoa kilimanjaro.

Dennis zacharia shemtoi ni mkurugenzi wa dawati la ufindi katika kikosi cha waombolezaji wa timu ya Arusha all stars ya jijini arusha amesema kuwa kila ifikapo August nane huadhimisha siku hiyo kwa kuwa kumbuka wenzao waliopata ajali ya Gari mnamo mwaka 1990.

Amesema katika kuwaenzi veteran's Hao kamati ya uongozi wa Krabu ya arusha all stars pia wameandaa bonanza maalumu kwa ajili ya kushiriki katika michezo bonanza litakalo husisha mchezo wa kabumbu kwa maveteran mbalimbali. 

Kwa upande wake kocha anaekinoa kikosi Cha maveteran wa Arusha all stars Azizi Nyoni amesema kuelekea bonanza hilo mpaka Sasa kikosi chake kiko Sawa kwa ajili ya mapambano ambapo pia kocha Azizi akatumia fursa hiyo kutoa rai kwa wachezaji vijana kuwa na nidhamu na bidii katika mchezo wa  soka kwa ajili ya kujijengea nja ya kuitangaza Tanzania katika soka la kulipwa. 
Maveteran Hao wanataraji kuungana kwa pamoja kwa ajili ya kuwaombea dua wenzao walio Pata ajali na kupoteza maisha mkoani kilimanjaro ambapo Tarehe Sita mwezi wa nane watadhuru makaburi ya wenzao kabla ya kushuka dimbani siku ya Tarehe nane. 

Kwa mujibu wa mkurugenzi wa bench la ufindi bwana Dennis Zacharia miongoni mwa walio poteza maisha katika ajali hiyo ni amani mwalimu, Judicate EStomihi, pamoja na Francis Lungu.
Mula Ametoa Mola ametwa Jina Lake litukuzwe. Amen.

 

 






 
 

No comments