KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI YATOA TAARIFA
ARUSHA
Kamati ya maadili ya madiwani ambayo ilikuwa imepewa
jukumu la kufuatilia malalamiko ya diwani wa kata ya Mwandeti Bwana Boniface
Tarakwa akimlalamikia Mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha DC Bwana Naoh Lembris
imetoa taarifa yake kuhusu walioyabaini.
Wakieleza mbele ya kikao cha baraza la madiwani kamati
hiyo ilipokea malalamiko kutoka kwa Bwana Boniface kwamba mwenyekiti wa
halmashauri amemwita mnafiki na anapaswa kuombewa katika mkutano wa baraza .
Hata hivyo kamati hiyo ilipokea malalamiko ya mwenyekiti
wa halmashauri Bwana Noah Lembris akimlalamikia Mh Boniface Tarakwa kumdhalilisha
kwenye mkutano na hadhara kitongoji cha Ekenywa kwa kusema alitumia fedha za
mradi wa maji shilingi milioni sitini jambo ambalo si ukweli.
Wakieleza hatua zilizofikia dhidi ya Mh Boniface Taraka
pamoja na Mh Noah Lembris kuhusu maneno ya kashfa amesema kuwa Menyekiti ametiwa
hatiani kwa kosa la kutoa maneno ya kashfa na ametoa neno lisilo na staha (MNAFIKI)
na muongo na anapaswa kwenda kuombewa.
Hata hivyo kuhusu suala la mwenyekiti wa halmashauri
kuema Mh Boniface Tarakwa ndiye anayezuia kata ya mwandeti isigawanywe jambo lililojitokeza katika ziara ya mbunge
wa Arumerukamati hiyo imeona hakukuwa na maeno ya uchochezi ala udhalilishaji
kani lilikua ni ukumu lake katika kusimamia ugawaji a kata hiyo.
Wakitoa maamuzi mbele ya baraza la madiwani Kamati hiyo
ya maadili kulingana na kanuni na tangazo la serikali kinalohusu madiwani namba
280 la tarehe 4 agosti 2000 wamesema kifungu cha 35 (c) kimetoa kimetoa adhabu
ambazo zinaweza kutolewa kwa diwani ambaye ametiwa hatiani ka kuvunja kanuni za
maadili a madiwani.
Wakielezea adhabu hizo wamesema diwani akitiwa hatiani
anatakia kupewa kwa mara ya kwanza na ya
pili,Kumshitaki Diwani pamoja na kuweka taarifa za diwani huyo katika ripoti ya
uajibikaji ya halmashauri nzima hivyo anatakiwa kupewa adhabu kwa mujibu wa
kanuni hizo.
No comments