SIMBA YAIBUKA KIDEDEA DHIDI YA MADINI FC


Mashabiki wa timu zote mbili waliwa katika uwanja wa Shekhe Amri Abeid Uliopo jijini Arusha .Picha na Vero Ignatus  Blog.Timu zote mbili Simba SC pamoja na Madini  SC ,wakiwa wanaingia uwanjani tayari kwa mpambao,Picha na Vero Ignatus Blog
Baadhi ya mashabiki wa timu zote mbili wakisubiria mechoi iaza.Picha na Vero Ignatus Blog                  

Na.Vero Ignatus Arusha.

Club ya soka ta simba imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya kombe la shirikisho Tanzania baada ya kuilaza Madini ya Arusha bao moja Kwa bila

Koncha msaidizi wa simba Jackson Mayanja amewashukuru wapenzi wa Simba Kwa kujitokeza Kwa wingi  kuliko vile ambavyo walikuwa wanategemea.


Mayanja amesema kiwa changamoto kubwa waliyokumbana nayo katika mchezo huo ni pamoja na hali ya uwanja in mbovu hauna nyasi za kutosha jambo ambalo limepelekea Simba kukosa mabao mengi.

Aidha Goli hilo lililoipa simba ushindi  lilifungwa kipindi cha pili  na  Loudit Mavungo (11)dakika ya 60.


Mayanja amesema kesho wanakwenda kucheza mchezo wa kirafiki mererani ambapo hakutaja watachacheza mechi hiyo na timu ipi ambapo wakimaliza jumanne wataanza safari kurudi Dar es salaam.


Kwa upande wake kocha wa timu tya Madini Fc Abdallah Juma amesema kuwa timu yake ipo vizuri japo kuwa wamefungwa goli moja lakini Vijana wameonyesha uwezo walionao na huu ni mwanzo mzuri kwao.


Aidha katika mtanange huo mchezaji wa timu ya simba  Ibrahimu Ajibu katika kipindi cha kwanza dakika ya 34 alipewa kadi ya manjano.

No comments