KITAIFA Watuhumiwa wa makosa ya ugaidi wamesema hawatahudhuria tena mahakamani

Na,Vero Ignatus,Arusha.

Watuhumiwa hao 61 wa makosa ya Ugaidi Arusha  mapema leo asubuhi walimuhakikishia Hakimu Nestory Banda kuwa tarehe 11/04/2017, Hawatahudhuria tena  mahakamani hapo hadi  upeleezi utakapokamilika.

" Ni zaidi ya miaka minne sasa kila tukija mahakamani hapa mnatuambiwa kuwa upelelezi haujakamilika ,hata R.C.O alivyokuja kutuona mwezi wa kwanza mwaka huu alituahidi kuwa ndani ya miezi miwili upelelezi utakuwa umekamilika sasa tunashangaa mpaka sasa hivi hakuna lolote linaloendelea"

Hakimu anaendesha kesi hiyo Nestory Banda amewaambia watuhumiwa  hao siku ya tarehe 11 ni lazima wahudhuria mahakamani .

"Nawaaahidi  kwamba mara baada ya kumaliza shughuli za ki Mahakama  kwa leo nitampigia simu R.C.O wala msiwe na taabu nyie njooni mahakamani "

Pichani ni baadhi ya watuhumiwa  walivyowasili Mahakamani.

Gari iliyobeba mahabusu wa kesi ya ugaidi likiondoka Mahakamani kuelekea gereza kuu la Arusha 

No comments