Ajali Mbaya ya Lori lililobeba mawe, Laua Mtu Mmoja
Makete
Lori
lililokuwa limebeba mawe limepinduka katika kijiji cha Masisiwe na
kusababisha majeruhi na kifo cha mtu mmoja ambaye alikuwa katika lori
hilo
Taarifa
za awali kutoka eneo la tukio zinasema kuwa lori hilo limepoteza
muelekeo ghafla kisha likaanza kupinduka kwa kubiringika mara kadhaa
umbali unaokadiriwa kuwa zaidi ya mita 80 kutoka barabarani
Ajali hiyo inadaiwa kutokea kati ya saa nane na saa tisa alasiri hii leo
Baadhi
ya mashuhuda waliokuwa eneo la tukio ambao hawakutaka kutaja majina yao
wamesema Lori hilo lilikuwa linatoka kubeba mawe kwa ajili ya kujenga
daraja katika kata ya Ipepo ndipo lori hilo lilipopoteza mwelekeo likiwa
njiani na kupinduka kisha kuporomokea bondeni
Jeshi la polisi Makete limefika eneo la tukio na kuuchukua mwili wa marehemu kwa uchunguzi zaidi
Tutawaletea taarifa kamili ya tukio hilo pindi mamlaka husika zitakapatia
Polisi wakipima jinsi ajali hiyo ilivyotokea
Askari Polisi akiangalia mawe yaliyokuwa yamebebwa na lori hilo kabla ya kutokea ajali
Mwili wa marehemu ukiingizwa kwenye gari
Mwili wa marehemu ukiwa ndani ya gari la polisi
Lori hilo likionekana kwa mbali baada ya ajali
Muonekano wa lori hilo baada ya ajali
Ajali ilipoanzia, hapa ndipo lori hilo lilipotumbukia
habari/picha na Edwin Moshi wa Eddy Blog






















No comments