Breaking news,Lawrence Masha ajiengua kugombea nafasi ya urais TLS

Mgombea wa kiti cha urais  Chama cha wanasheria Tanganyika(TLS) Lawrence Masha ametengua uamuzi huo na kusema kuwa  ameamua kuumuunga mkono mgombea mwenzake Tundu Lissu.

Maamuzi hayo ameyafanya wakati alipokaribishwa ili kujieleza katika mkutano unaoendelea katika kituo cha mkutano cha kimataifa Aicc Jijini Arusha Leo.

Aidha mwenyekiti wa uchaguzi amesema kuwa Kwa kuwa Lawrence Masha siyo mgombea tena haruhusiwi kuulizwa maswali tena.

No comments