Mpinga asema: Tanzania imepata mafanikio makubwa katika kuthibiti ajali za barabarani.
| Kamanda wa kikoai cha usalama wa barabarani DCP Mohamed Mpinga akizungumza katika hafla ya kufunga kampeni ya Abiria Paza Sauti iliyofanyika katika kituo cha mabasi yaendayo mikoani na nchi jirani cha Ubungo, ambapo kampeni hiyo ilizinduliwa Novemba 2016 na Naibu waziri wa mambo ya ndani Mh. Hamad Masauni ambaye pia ni mwenyekiti wa baraza la usalama barabarani Tanzani. |
Na. Vero Ignatus & Murtadhwa Elbahsan Dar es salaam.
Madereva
wa mabasi makubwa yaendayo mikoani wameaswa kutokuchezea mfumo wa
kufuatilia mwenendo wa mabasi haswa mwendo kasi ,yeyote atakae bainika
ameuharibu hatua kali za kisheria zichukuliwe dhidi yake.
Hayo
yamesemwa na Kamanda wa kikosi cha usalama barabarani nchini Mohamed
Mpinga katika hafla ya kufunga kampeni ya abiria paza sauti
iliyofanyika katika katika kituo cha mabasi yaendayo mikoani na nchi
jirani cha Ubungo ambapo amesema kuwa mwendo kasi ni chanzo kikubwa cha
ajali barabarani
Kamanda
amefafanua kuwa kampeni hiyo imeleta matokeo chanya ambayo imeonyesha
kupungua kwa ajali ukilinganisha na miaka 25 iliyipita nakusema kuwa
Tanzania imepata mafanikio makubwa katika kuthibiti ajali za barabarani .
Amezitaja
takwimu hizo kuanzia mwaka 2015 Desemba ajali zilikuwa 767 , Disemba
2016 ajali zilikuwa 705, ambapo januari 2016 ajali zilikuwa 681 hadi
januari 2017 ajali zilikuwa 525, Februari 2016 ajali zilikuwa 846 ambapo
februari 2017 ajali zilikuwa 455 ,kuna upungufu wa asilimia 46 'ambapo
ajali zinazidi kupungua mwaka hadi mwaka.
Ameendelea
kusema kuwa kwa takwimu hizo hadi sasa Tanzania imepiga kubwa katika
kudhibiti ajali za barabarani na hii ni takribani nusu karne tangia
mwaka 1989.
Vile
vile Kamanda mpinga alitoa vyeti vya pongezi kwa madereva walio
pendekezwa kama madereva bora kwa mwaka 2016 - 2017 ambao ni;
1. AWADH BAWAZIR(RATCO).
2.ALLY ISSA (STAR BUS)
3. MUSTAPHA GHARIB(KIMBINYIKO)
4. DAUDI LWENA(KHANDAHAR).
1. AWADH BAWAZIR(RATCO).
2.ALLY ISSA (STAR BUS)
3. MUSTAPHA GHARIB(KIMBINYIKO)
4. DAUDI LWENA(KHANDAHAR).
5. MENGI KASIKE(SUTCO).
6. MAJURA KAFUMU
6. MAJURA KAFUMU
Kwa
upande wake mratibu na mwenyekiti wa abiria paza sauti Asp.Mosi Ndozero
amesema kuwa wamekuwa wakitoa elimu kwa madereva pamoja na wahudumu wa
magari sambamba na kuwaelimisha abiria kufahamu haki zao pia kutoa
taarifa kwa jeshi la polisi pale wanapoona viashiria vya uvunjifu wa
sheria za barabarani ambavyo vinaweza kusababisha ajali na kupoteza
maisha au ulemavu wa kudumu.
Mosi
amesema kuwa mtu anapopata ajali haathiriki yeye peke yake inajumuisha
familia yake pamoja na serikali kuingia gharama kubwa ya kumuuguza huyu
mtu aliyepata ajali,amewataka mabalozi kuendelea kupaza sauti kwa
madereva bodaboda ambao wanapakiza mizigo kuzidi uwezo wa pikipiki
pamoja na wale anaopakia Mishikaki.
Picha na Vero Ignatus & Murtadhwa Elbahsan
![]() |
| Askari wa uaslama barabarani wakiwa katika picha ya pamoja na kamanda wa usalama barabarani Mohamed Mpinga mara baada ya kufungwa rasmi kwa kampeni hiyo. |
Dereva awadhi ramadhani ambae ameanza kuendesha magari kuanzia mwaka 1970 na kampuni ya Scandinavia nabaadae kuhamia kampuni ya Ratco akipokea cheti kutoka Kamanda wa kikosi cha usalama barabarani Mohamed Mpinga
Kamanda wa kikosi cha usalama barabarani Mohamed Mpinga akimkabidhi cheti mwandishi wa habari wa kituo cha ITV ,Monyo kwa niaba ya kituo hicho ka kutoa mchango mkubwa katika kampeni ya paza sauti . Madereva bora wa 2016-2017 wakiwa katika picha ya pamoja na Kamanda wa kikosi cha usalama barabarani Mohamed Mpinga.
Balozi wa usalama barabarani Elizabeth Maembe akikabidhiwa cheti na kamanda wa Usalama barabarani nchini Mohamed Mpinga
Mwenyekiti waumoja wa madereva (UWAMATA)aliyeshika simu akiwakilisha umoja huo katika hafla hiyo ya kufunga kampeni ya abiria paza sauti
Mwenyekiti wa Mabalozi wa usalama barabarani (RSA) John Seka akizungumza katika hafla hiyo.
Makamu mwenyekiti wa mabalozi wa usalama barabarani Irene Mselem akipokea cheti kutoka kwa kamanda wa usalam barabarani katika ufungaji wa kampeni ya abiria paza sauti











No comments