GUGU HATARI UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA NAIROBI (JKIA)
Na.Vero Ignatus .Arusha.
Gugu hatari la mmea unaodaiwa kupatikana katika
maeneo machache hapa nchini Tanzania unajulikana
kama 'Gugu karoti' kwa kitaalamu 'Parthenium hysterophorus' umeonekana
katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta nchini Kenya.
Akinukuliwa
habari hizi, mtaalamu mshauri wa Shirika la ECHO
ukanda wa Afrika Mashariki ndugu Charles Bonaventure (Bonny), amesesema,
“ni
kweli kwamba gugu hili nimeliona uwanja wa ndege wa kimataifa wa Nairobi
asubuhi ya tarehe 30/04/2017,Ambapo amesema kuwa ni hatari kama jitihada ya kulitokomeza hazitachukuliwa kwa haraka litaendelea kuzagaa.
" Changamoto kubwa nayoiona ni
uelewa wa majani haya, hivyo elimu na
uhamasishaji wa majani haya ni muhimu kutolewa kwa jamii”
Aliendelea kusema gugu
hili
limezagaa njia nzima ya kutokea Nairobi mjini hadi sehemu za Kajiado na
kwa
upande wa Tanzania ameliona zaidi maeneo ya Ngaramtoni, Kwa Mrombo na
Njiro. Pia limepamba barabara mpya inayojengwa inayotokea Sakina hadi
Tengeru.
Hivi karibuni mwandishi wa blog hii alikutana na mwananchi huyu ambaye hakupatikana jina lake mara moja amejipamba majani haya kwa ajili ya jambo alilokuwa analisheherekea kama unavyoona katika picha.
Majani ya gugu karoti ni hatari kwa afya za binadamu,
wanyama na mimea.
Kwa habari zaidi soma: https://ignatusvero.blogspot.c om/2017/04/ufahamu-mmea-wa-gug u-karoti-na-madhara.html
No comments