Waziri wa Fedha na Mipango akutana na viongozi wa IMF na balozi wa Hungary

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) anaeziwakilisha nchi 23 za Afrika, Bw. Maxwell Mkwezalamba (wa pili kulia) akieleza kuwa Tanzania inakua kwa kasi kiuchumi jambo ambalo linawavutia viongozi wengi kufuatilia kwa karibu maendeleo yake, alipokutana na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (kushoto), katika Ukumbi wa Wizara Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), akiongoza Mkutano kati yake na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) anaeziwakilisha nchi 23 za Afrika, Bw. Maxwell Mkwezalamba (mbele kulia) ambapo alisema mahitaji makubwa wa nchi ni maendeleo ya kilimo na upatikanaji wa nishati ya umeme ili viweze kuchochea uchumi wa viwanda. Mkutano huo umefanyika katika Ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) anaeziwakilisha nchi 23 za Afrika, Bw. Maxwell Mkwezalamba ( kulia) wakipeana mkono baada ya kumalizika kwa Mkutano kati yao uliohusu suala la Uchumi katika Ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango jijini Dar es salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (watatu kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) anaeziwakilisha nchi 23 za Afrika, Bw. Maxwell Mkwezalamba (wa tatu kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na Viongozi na Maafisa waandamizi wa Wizara hiyo baada ya kumalizika kwa mkutano kuhusu hali ya uchumi katika Ukumbi wa Wizara Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wajumbe wa Mkutano kati ya Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) anaeziwakilisha nchi 23 za Afrika, Bw. Maxwell Mkwezalamba (hayupo pichani) wakimuaga baada ya kumalizika kwa Mkutano katika ukumbi wa Wizara hiyo Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (wa tatu kulia) akielezea mpango wa Serikali wa kuboresha kilimo ili kukuza uchumi wa viwanda alipofanya Mkutano na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Tao Zhang (wa tatu kushoto), katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango jijini Dar es salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (kushoto) akielezea kuhusu ujenzi wa Reli kwa kiwango cha Kimataifa (Standard Gauge) ambapo alisema itasaidia kuchochea maendeleo si tu kwa Tanzania bali na nchi jirani, wakati wa Mkutano na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Tao Zhang (hayupo pichani) katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Prof. Benno Ndulu.
Naibu Mkurugenzi wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Tao Zhang (kushoto) akizungumza na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (hayupo pichani) kuhusu nia ya Shirika hilo kufungua fursa zaidi za mikopo kwa Tanzania, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (wa nne kushoto) na Naibu Mkurugenzi wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Tao Zhang (wa nne kulia) wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumalizika kwa Mkutano kati yao katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango jijini Dar es salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (kulia) na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Tao Zhang (kushoto) wakiagana baada ya kumaliza mkutano kati yao, katika Mkutano huo Zhang aliipongeza Serikali kwa hatua nzuri za ukuaji wa Uchumi.
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Prof. Benno Ndulu (kulia) akipeana mkono na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) anaeziwakilisha nchi 23 za Afrika, Bw. Maxwell Mkwezalamba (kushoto) baada ya kumalizika kwa Mkutano kati ya Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Tao Zhang katika Ofisi za Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es salaam
Balozi wa Hungary hapa nchini mwenye makazi yake Nairobi Kenya, Laszlo Mathe (kushoto) akionesha nia ya nchi yake kuwa na ushirika wa maendeleo na Tanzania utakao wezesha nchi hizo mbili kunufaika kiuchumi kupitia Sekta mbalimbali za Maendeleo, wakati wa Mkutano kati yake na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (hayupo pichani), katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango jijini Dar es salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (kulia) akizungumza kuhusu fursa zilizopo za uwekezaji katika Nishati, Miundombinu, Kilimo wakati wa Mkutano kati yake na Balozi wa Hungary hapa nchini mwenye makazi yake Nairobi Kenya, Laszlo Mathe (kushoto), katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango, Jijini Dar es salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (kushoto) akipongezana na Balozi wa Hungary hapa nchini mwenye makazi yake Nairobi Kenya, Laszlo Mathe (kulia), baada ya kumalizika kwa Mkutano kati yao kuhusu uwekezaji wenye tija kwa pande zote mbili. Mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (kushoto) na Balozi wa Hungary hapa nchini mwenye makazi yake Nairobi Kenya, Laszlo Mathe (wa pili kushoto), wakibadilishana mawazo na wajumbe wengine walihudhuria mkutano kati yao kuhusu uwekezaji wenye tija, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es alaam.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (kulia) na Balozi wa Hungary hapa nchini mwenye makazi yake Nairobi Kenya, Laszlo Mathe (kushoto) wakiagana baada ya kumalizika mkutano kati yao ambapo Balozi huyo ameonesha nia ya nchi yake kuwekeza nchini. Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini - Wizara ya Fedha na Mipango













No comments