UFUNGUZI WA MKUTANO MKUU WA MWAKA WA SARPCCO WAFANYIKA JIJINI ARUSHA LEO.





Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya ndani ya nchi, Mhe.Hamad Masauni akizungumza na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu wakati anawasili katika ukumbi wa mikutano wa AICC kwa ajili ya ufunguzi wa Mkutano mkuu wa mwaka wa Shirikisho la Wakuu wa Polisi kutoka nchi za kusini mwa Afrika (SARPCCO). Kulia ni Mkuu wa INTERPOL kanda ya Kusini Mubita Nawa.( Picha na Hassan Mndeme-Jeshi la Polisi)


Katibu Mtendaji wa SADC, Dk.Stegnomena Tax akizungumza na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu kabla ya ufunguzi wa Mkutano mkuu wa mwaka wa Shirikisho la Wakuu wa Polisi kutoka nchi za kusini mwa Afrika (SARPCCO) unaofanyika mkoani Arusha. IGP Mangu ndiye Mwenyekiti wa shirikisho hilo kwa kipindi hiki. Picha na Hassan Mndeme-Jeshi la Polisi)


Baadhi ya Wakuu wa majeshi ya Polisi kutoka nchi za kusini mwa Afrika SADC wakitoa heshima wakati wimbo wa taifa unapigwa wakati wa hafla ya ufunguzi wa Mkutano mkuu wa mwaka wa Shirikisho la Wakuu wa Polisi kutoka nchi za kusini mwa Afrika (SARPCCO) uliofanyika Mkoani Arusha. IGP wa Tanzania, Ernest Mangu ndiye Mwenyekiti wa shirikisho hilo kwa kipindi hiki. Picha na Hassan Mndeme-Jeshi la Polisi)
 


Katibu Mtendaji wa SADC, Dk.Stegnomena Taxi, akitoa hotuba wakati wa hafla ya ufunguzi wa Mkutano mkuu wa mwaka wa Shirikisho la Wakuu wa Polisi kutoka nchi za kusini mwa Afrika (SARPCCO) Mkutano huo ulifunguliwa na Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya ndani ya nchi, Mhe.Hamad Masauni Mkoani Arusha. IGP wa Tanzania Mangu ndiye Mwenyekiti wa shirikisho hilo kwa kipindi hiki. Picha na Hassan Mndeme-Jeshi la Polisi)


Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya ndani ya nchi, Mhe.Hamad Masauni akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Polisi kutoka nchi za kusini mwa afrika (SARPCCO) baada ya ufunguzi wa Mkutano mkuu wa mwaka wa Shirikisho la Wakuu wa Polisi kutoka nchi za kusini mwa Afrika unaofanyika Mkoani Arusha. Picha na Hassan Mndeme-Jeshi la Polisi.
 
Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini,  IGP Ernest Mangu akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) akiwa ameambatana na Mkuu wa Jeshi la Polisi la Angola, Paulo de Almeida (kushoto) na Mkuu wa jeshi la Polisi la Msumbiji, Paulo Chachine (kulia) wakati wa Mkutano mkuu wa mwaka wa Shirikisho la Wakuu wa Polisi kutoka nchi za kusini mwa Afrika (SARPCCO) uliofanyika Mkoani Arusha.(Picha na Hassan Mndeme-Jeshi la Polisi.


Na.Vero Ignatus ,Arusha. 
 

Mkuu Wa jeshi la Polisi Nchini Tanzania  IGP Ernest Mangu amekuwa umoja unaounda nchi zilizopo kusini mwa Africa (SARPCO )zitahakikisaha kuwa zinaimarisha swala la ulinzi na usalama ili kuweza kuleta maendeleo katika nchi 15 zinazounda umoja huo.

Ameyasema hayo katika  ufunguzi wa Mkutano mkuu wa mwaka wa Shirikisho la Wakuu wa Polisi kutoka nchi za kusini mwa Afrika (SARPCCO) ulioshirikisha nchi 15 zilizounda umoja,ambao umefanyika katika kituo cha kimataifa cha mikutano (AICC) uliopo mkoa Wa Arusha.

IGP Mangu amesema kuwa lengo la Mkutano huo nikuendeleza mashirikiano kati ya nchi hizo ,ualifi unaovuka mipaka ,udhibiti Wa madawa za kulevya,ambazo zimekuwa ni changamoto kubwa Pamoja na uharamia.

"Umuhimu siyo tu kushirikiana bali ni kutumia mbinu mbadala za Teknolojia za kisasa ili kubadilishana taarifa za kutimiza malengo hayo" alisema Mangu.

Katubu mtendaji wa SADC 
Dk.Stegnomena Tax amesema kuwa amezungumzia suala LA kuweka mikakati na Sera za kuwa pamoja na kujipanga ili kuweza kutokomeza biashara haramu ya kusafirisha binadamu haswa mama na mtoto.

"Hali yeyote ya kupambana na uhalifu lazima ushirikiane na nchi za jirani peke yako huwezi kutokomeza sawa za kulevya,biashara haramu ya binadamu,usafishaji Wa fedha,kuhakikisha mazingiravyetu yapo salama,na kukomesha uharamia"alisema Katibu mtendaji Wa SADC.


Naibu waziri
Wa Mambo ya ndani Injinia Ahamad Masauni amezitaka nchi hizo za  (SARPCCO)washirikiane kimalengo,kimkakati,na kuhakikisha majeshi ya nchi hizo yanakuwa ya kisasa,wafanye mafunzo kwa pamoja kwa kubadilishana taarifa.

" Tatizo la biashara haramu ya kusafirisha Binadamu siyo kwa SADC peke yake ,bali ni tatizo linaloikumba dunia nzima kama takwimu zinavyoonyesha"alisema Masaun
i.



No comments