WAAJIRI WAPEWA SIKU 30 KUFIKISHA MICHANGO YA WATUMISHI WAO.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dr.Ashatu Kijaji akifungua mkutano mkuu
wa nane wa wadau wa mfuko wa mafao ya kustaafu wa GEPF uliofanyika Jijini Arusha na kuhudhuriwa na wadau wa mfuko.Picha na Vero Ignatus Blog.
Mkurugenzi mkuu wa mfuko huo Daud Msangi akizungumza katika mkutano wa nane wa Wadau wa mfuko wa Mafao ya kustaafu wa GEPF ,,leo Jijini Arusha .Picha na Vero Ignatus Blog.

Mwenyekiti
wa bodi ya GEPF Joyce Shaidi akizungumza katika mkutano huo ambapo
amesema kuwa kauli mbiu ya mkutano huo ni "Hifadhi ya jamii kwa wote
inawezekana katika uchumi wa viwanda"kauli mbiu hii imewekwa maksudi na
kumuunga mkono Rais katika kujenga uchumi wa viwanda.Picha na Vero Ignatus Blog
Katibu
Tawala Mkoa wa Arusha Richard Kwitega akiongea katika mkutano huo
ambapo alimuakilisha mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo .Picha na Vero Ignatus Blog

Mtendaji mkuu Benki ya Posta Sabasaba Moshingi akitoa neno la shukrani katika mkutano huo.Picha na Vero Ignatus Blog.
Kulia ni mtendaji mkuu wa UTT James WAshima akizungumza katika mkutano huo pembeni ni Mkurugenzi mkuu wa GEPF Daud Msangi
Wadau katika mkutano wakifatilia mada mbalimbali

Naibu waziri wa Fedha na Mipango Dr.Ashatu Kijaji akizindua mpango wa gharama nafuu utakao wahudumia watu wote waliojiunga na mfuko huo.Picha na Vero Ignatus Blo.
Picha ya pamoja.
Naibu waziri wa Fedha na Mipango Dr.Ashatu Kijaji akizindua mpango wa gharama nafuu utakao wahudumia watu wote waliojiunga na mfuko huo.Picha na Vero Ignatus Blo.
Naibu waziri
wa fedha na mipango Dkt Ashatu Kijaji ameziagiza bodi za mifuko ya hifadhi ya
jamii nchini katika kutekeleza majukumu yao kwa kufata sheria zilizopo kuwabana
waajiri wa kampuni na taasisi mbalimbali kwa lengo la kuleta maendeleo ya taifa
na faida kwa wanachama na watakao kaidi wafikishwe mahakamani kwa mujibu wa
sheria.
Akizungumza katika
mkutano mkuu wa nane wa wadau na wanachama wa mfuko wa mafao wa GEPF Dkt Ashatu
amesema sheria zipo wazi hivyo ni vyema viongozi wa mifuko kufata sheria ili
kudhibiti uzembe unao endele kwa baadhi ya kampuni.
"Kama serikali ilikuwa inadaiwa na tayari imeshalipa shilingi bilioni 249 kiasi kilichosalia cha bilioni 35 kitakamilishwa ikifikapo 31juni 2017."alisema Kijaji
Bi Joyce
Shaidi ni mwenyekiti wa bodi ya mfuko wa mafao wa GEPF akatumia fursa hiyo
kupiga vita suala la matumizi ya madawa ya kulevya katika kuelekea Tanzania ya
viwanda kwani nguvu kazi kubwa ya uzalishaji ni kwa vijana kwa maslahi ya
taifa.
"Hadi sasa mfuko huu una jumla ya wanachama 1,14,462 pesa zilizopo kwenye mfuko kwa sasa ni shilingi Bilioni 428.09 tunatazamia ifikapo june 2017 mfuko utakuwa na bilioni 505,tunatarajia ifikapo 2020 mfuko utakuwa na trilioni 1"alisema mwenyekiti huyo.
Edward Nzota
na Janeth Asajile ni miongoni mwa washiriki katika mkutano huo na mwanaeleza umuhimu wa kulipia michango ya mifuko ya hifadhi.
| |||

No comments