WASHIRIKI WA KILLI MARATHON KUNUFAIKA NA TIGO 4G

Displaying IMG_0511.JPG
Mkurugenzi wa Kampuni ya Mawasiliano ya Tigo kanda ya Kaskazini George Lugata (kulia) akionyesha laini ya 4G internet zitakazotumika kwenye mashindano ya Killi Marathon yaliyodhaminiwa na Kampuni hiyo.Kushoto ni Meneja Mauzo wa Tigo Moses Busee.Picha na Ferdinand Shayo

Na Ferdinand Shayo,Arusha.

Kampuni ya Simu ya Tigo Imejipanga kuhakikisha kuwa huduma za mtandao wa 4G inapatikana kipindi chote cha Mashindano ya riadha ya kimataifa ya Killi Marathon yanayotarajia kufanyika Februari 26 mwaka huu katika mkoa wa Kilimanjaro.

Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Kaskazini George Lugata amesema kuwa kampuni hiyo itatua mtandao wa kasi  ya ajabu ya 4G katika Mkoa wa Kilimanjaro na viunga vyake katika jitihada za kuhakikisha Washiriki wa mbio hizo wanafurahia huduma zao.

Lugata amesema kuwa kuboreshwa kwa huduma hizo kunatoa fursa kwa wafanyabiashara na watalii katika mkoa wa Arusha kunufaika na fursa ya Mawasiliano inayotolewa na Tigo.

“Wakazi wa Moshi watakaokuja kwenye mashindano wataweza kutumia vizuri mitandao ya kijamii kama facebook,watsap,skype na mingine mingi na kufurahia kutuma picha katika mitandao” Alisema

Pia Washiriki wa Mbio hizo wataweza kujipiga picha na kuzituma kwa watu wanaowapenda kama njia mojawapo ya kuwajulisha watu kuhusu mashindano hayo.

Alisema kuwa kampuni hiyo imejizatiti na kuongeza idadi ya minara ya simu ili kukuza na kuboresha huduma za simu.

Lugata amewataka Wakazi wa Kilimanjaro na mikoa yote ya Tanzania kujitokeza katika Mashindano hayo ya kusisimua ndani na nje ya nchi.

No comments