SERIKALI IWASHIRIKISHE WAFANYABIASHARA KUPIGA VITA RUSHWA
Na Mwandishi Wetu,Pwani
SERIKALI
imeombwa kushirikiana na asasi za kiraia pamoja na makampuni ya kibiashara yaliyopo nchini katika
kupiga vita vitendo vya rushwa na badala yake iache kusubiri msaada wa fedha
kutoka kwa wafadhili.
Mkurugenzi
wa asasi ya kitaifa ya Maendeleo ya Vijana (YPC) Israel Ilunde,alitoa kauli
hiyo jana wakati akizungumza kwenye jukwaa la ufahamu wa kiraia lililofanyika
Mjini Kibaha na kuwashirikisha wananchi pamoja na viongozi mbalimbali.
Ilunde,alisema
kuwa suala la rushwa bado ni changamoto kubwa hapa nchini japo limekuwa
likipigwa vita kali na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Magufuli
lakini pekee hatoweza bila kumpa ushirikiano.
Alisema
kuwa,umefika wakati muafaka wa Serikali kukaa pamoja na makampuni ya kibiashara
pamoja na asasi za kiraia ili kuweka misingi imara itakayosaidia kukomesha
jambo hilo kuliko kusubiri watu wa nje waje kutusaidia.
Ilunde,alisema
kupiga vita suala hilo linahitaji uzalendo wa wananchi wenyewe ambao watasimama
katika kukemea vitendo vya rushwa na kwamba kusubiri fedha za wafadhili ni wazi
kuwa hatutaweza kufikia malengo.
“Mimi
nasema,tusiendelee kupokea fedha kutoka nje ili tupige vita rushwa lakini
tunaweza kukomesha rushwa kwa kuwatumia wananchi wenyewe ambao ni wazalendo wa
nchi yao wanaoweza kusimama na kupiga
filimbi juu ya janga hili,”alisema Ilunde.
Aidha
,Ilunde aliishauri Serikali kuhakikisha inatengeneza sheria ambayo itakuwa
inawalinda watoa taarifa za rushwa ambapo hatua hiyo itawasaidia wananchi
kuondoa hofu na hivyo kutoa ushirikiano
mzuri kwa Takukuru.
Hata hivyo,Ilunde
alizitaka asasi za kiraia zilizopo nchini kuendelea kutoa elimu ya uraia kwa
jamii ili waweze kufahamu madhara ya rushwa licha ya kuwa hawawezi kufanyakazi
ya Takukuru lakini watasaidia kuelimisha jamii dhidi ya mapambano hayo
| |||

No comments