SERIKALI ya Ujerumani imetoa Euro milioni 20.5 kwa ajili ya mradi wa kutekeleza Maendeleo mbalimbali ya wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti na Ngorongoro.

Aidha fedha hizo zitawezesha uboreshaji wa miundo mbinu ya Ecosystem ya Serengeti maarufu kwa jina la "Serengeti Ecosystem Devolopment and Conservation Project (SEDCP)"

Akizungumza  kwenye ofisi za TANAPA wakati wa kusaini mkataba wa mradi huo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Serengeti Juma Keya alishukuru Ujerumani kuwapatia fedha hizo zitakazofanikisha kukuwa kwa maendeleo ya wananchi waliopo pembeni mwa Hifadhi za Serengeti na Ngorongoro.

Amesema baadhi ya shughuli zitakazotekelezwa na mradi huo ni pamoja na sekta ya Elimu, Afya,maji safi,Nishati ya sola,mifugo na ujenzi wa miundo mbinu ya barabara kwa Wilaya zote mbili.

"Mradi huu utawezesha wananchi kufika katika masoko na kupata huduma zingine za muhimu kwa kuwa na barabara safi, lakini kwenye Elimu kutakuwa na u jenzi wa nyumba za waalimu, maabara na mabweni,"alisema

Pia amesema kwenye sekta ya Afya wataboresha kwa kujenga Zahanati, nyumba za Madaktari na Manesi pamoja na ununuzi wa vifaa tiba,"alisema

Amewaomba wadau wa Ngorongoro kunisaidia mradi huo ufanikiwe badala ya kuingiza siasa.

Amesema mkataba huo umesainiwa na Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA), Halmashauri ya Serengeti na wajumbe wa serikali ya Ujerumani.

Hata hivyo wadau wa Halmashauri ya Ngorongoro wakiwakilishwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Ngorongori Methew Siloma  hawakusaini mkataba huo kwa madai mwaka wapate ufafanuzi wa mradi huo vizuri.

Naye Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Serengeti, Willium Mwakilema  alishukuru serikali ya Ujerumani na Taasisi zake kuamua kunisaidia Tanzania katika maeneo hayo.
Aliomba kuepuka wadau kuingiza siasa katika Uhifadhi ili mradi usikwame.

No comments