Mauaji ya mwanariadha yanaashiria nini kuhusu usalama wa wanawake nchini Kenya
Mauaji ya mwanariadha yanaashiria nini kuhusu usalama wa wanawake nchini Kenya

Mauaji ya mwanariadha Rebecca Cheptegei na mpenzi wake wa zamani yamezidisha wito wa kuchukuliwa hatua kali dhidi ya mauaji ya wanawake nchini Kenya.
Raia huyo wa Uganda mwenye umri wa miaka 33 alifariki siku chache baada ya kumwagiwa petroli na kuchomwa moto na mpenzi wake wa zamani nyumbani kwake katika kaunti ya Trans Nzoia magharibi mwa Kenya.
Lakini ifahamike kwamba hili sio tukio la pekee. Kenya ina moja ya viwango vya juu zaidi vya ukatili dhidi ya wanawake barani Afrika.
Ripoti za vyombo vya habari zinasema kuwa mwezi Januari pekee zaidi ya wanawake 10 nchini humo walikuwa wahanga wa mauaji ya wanawake, ambayo yameelezwa na Umoja wa Mataifa kama mauaji ya wanawake kwa sababu ya jinsia zao.
Jane, sio jina lake halisi, anaiambia BBC kwamba amekuwa mafichoni kwa kipindi kirefu tu cha mwaka.
Anasema hawezi kurejea kazini kutokana na majeraha yaliyobadilisha maisha yake aliyoyapata baada ya mpenzi wake wa zamani kuchomwa kisu kikatili.
“Nia yake ilikuwa kuniua. Alinichoma kisu na kuniacha nikiwa nimefariki dunia. Ikiwa si majirani, ningekuwa nimefariki,” Jane anakumbuka.
Anasema alivumilia miongo kadhaa ya unyanyasaji mbaya zaidi kabla ya kuondoka. Kilichomfanya kutoweza kuvumilia tena ni wakati alipoanza uchokozi wake kwa watoto, anasema.
"Kuishi naye ilikuwa kama kuwa kuzimu. Sijui nimewezaje kuvumilia kwa miaka hiyo yote,” Jane anaongeza.
Mume wake aliyeachana naye anaendelea kumnyanyasa.
“Naishi kwa hofu. Anasema anataka kunimaliza. Siwezi kulala usiku. Kwa sasa naendelea kupata tiba kusaidia afya yangu ya akili. Mimi sio mhalifu lakini naishi kama niko jela.”
Bbc
No comments