SIMANZI SIMANZI ,WANAFUNZI WANAFUNZI 33 WALIMU 2 NA DEREVA WAFARIKI KATIKA AJALI ..KARATU MKOANI ARUSHA
Basi la shule ya Lucky Vincent likiwa korongoni
Ajali mbaya ya gari imetokea kaskazini mwa Tanzania , ambapo basi aina ya Costa mali ya shule ya Lucky Vincent iliyoko eneo la kwa Mrombo ,limetumbukia katika mto Marera ulioko katika mlima Rhotia, , Karatu mkoani Arusha.
Mkasa huo umetokea takribani kilomita 25 kutoka katika geti la hifadhi ya taifa ya Ngorongoro ,takriban kilomita 150 kutoka mji wa Arusha.
Wanafunzi hao walikuwa wamesalia na kilomita 5 ili kufika sehemu waliokuwa wakielekea.
Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo Kamanda wa Polisi mkoani Arusha Charles Mkumbo amesema kuwa wanafunzi 33 wakiwemo walimu 2 pamoja na Dereva aliyekuwa anaendesha gari hilo.
Amesema kwamba dereva alidaiwa kutoijua barabara hiyo hivyobasi alikosa mweleko na kuteleza kando ya barabara kabla ya kutumbukia korongoni katika mto Malera.
Harakati za uokozi zikiendelea
Wananchi pamoja na wazazi wakiwa wamekusanyika katika shuleni hapo
Aidha maiti zimehifadhiwa katika hospitali ya Mkoa wa Arusha, Mount Meru.
Mkuu wa wilaya ya Arusha , Gabriel Daqqaro amewataka wananchi kuwa watulivu kutokana na tukio hilo baya, na kwamba serikali itatoa taarifa baadaye kuhusiana na msiba huo.
No comments