TBS: PIGA VITA BIDHAA HAFIFU
Na.Vero Ignatus Arusha.
Imebainika kuwa nchi ya Tanzania inakabiliwa na tatizo kubwa la uwo wa bidhaa duni na zenye viwango hafifu,ambapo tatizo hilo linanmadhara makubwa siyo tu kwa walaji au watumiaji wa bibdhaa au hudhuma hizo bali pia lina athari kubwa sana katika ukuaji wa uchumi wa nchi .

Mkuu wa Walaya ya Ngorongoro Rashid Taka ambaye amemuwakilisha mkuu wa mkoa wa Arusha katika mkutano wa majadiliano kuhusu uboreshaji wa utekelezaji wa matakwa ya viwango uliofanyika katika Kituo cha mikutano cha kimataifa (AICC) ukumbi wa Twiga.
Ameyasema hayo mkuu wa wilaya ya Ngorongoro Rashid Taka ambaye alikuwa amemuwakilisha mkuu wa mkoa wa ARusha Mrisho Mashaka Gambo.katika mkutano wa majadiliano kuhusu uboreshaji wa utekelezaji wa matakwa ya viwango uliofanyika katika Kituo cha mikutano cha kimataifa (AICC) na kuwashirikisha wadau mbalimbali wanaohusika katika utekelezaji na usimamiaji wa maswala yahusuyo utekelezaji wa matakwa ya viwango waliohudhuria mkutano huo.
Amesema kuwa upo umuhimu mkubwa wa wadau wa maswala ya viwango kufanya kazi kwa ushirikiano ili kuthibiti uzalishaji wa uwepo wa bidhaa duni nchini ,hivyo hatua ya kujadili na kukubaliana mikakati ya pamoja katika eneo hilo litaleta mazingira mazuri ya kiutendaji yasiyo na muingiliano au mgongano wa kimaslahiikiwemo pia kulinda mazingira hivyo kupata matumizi endelevu na kuiepusha jamii na athari za kiafya zitokanazo na utumiaji wa bidhaa duni zisizo na viwango.
"Jambo hili linahitaji ushirikishwaji mpana wa wadau katika upigaji vita upambanaji na uzalishaji wa bidhaa hafifu,hii ni vita yetu sote Watanzania wote kwa ujumla,inatakiwa hata mgeni anapokuja nchini mwetu atambue yakuwa sisi ni watu wa Viwango" alisisitiza Rashid mkuu wa wilaya ya Ngorongoro.
Akizungumza katika mkutano huo kaimu mkurugenzi wa Mamlaka ya kupima viwango vya ubora nchini ( TBS ) Dokta Egid Mabofu amesema kuwa lengo la kuwa na mkutano huu ni pamoja na kuwaleta wadau wa utekelezaji wa matakwa ya viwango hapa nchini ili kujadili mambo muhimu yanayohusiana na viwango,
" kufanya muendelezo wa meza ya majadiliano mkutano kama huu umeshafanyika katika mikoa mitatu ambayo ni pamoja na Dar-es salaam,Mtwara,Tanga na leo hii tupo Arusha kwa nia ileile hatuhitaji tena Nchi yetu iwe na bidhaa duni ambazo mwisho wasiku hupelekea madhara na kuathiri afya zetu" alisisitiza Mabofu.
Kwa upande wake wa muwakilishi wa Shirika la mazingira la Umoja wa
wa Mataifa (UNEP) CLara Makenya amesema kuwa hawakubaliani na bidhaa zisizokuwa na viwango ndiyo maana wao pamoja na Shirika linalosimamia viwango nchini Tanzania wameonelea kuwa na mkutano wa pamoja na Taasisi zote zinazojihusisha na kusimamia na kuthibiti viwango ili kupata suluhu juu ya uzalishaji wa bidhaa zisizokuwa na viwango ambazo pia zinaharibu mazingira kwa ujumla.
Aidha mkutano huo wa siku moja umewashirikisha wadau kutoka Mamlaka za usimamiaji wa viwango,Wizara mbalimbali,Polisi,Taasisi za elimu na Utafiti,Watumiaji wa huduma na bidhaa,wazalishaji wa bidhaa,Taasisi ya Sekta Binafsi nchini,Shirikisho la wafanyabiashara na Taasisi ukuzaji biashara.
Meneja viwango (Tbs) Mary Meela ambaye pia ni mratibu mradi akizungumza na wanahabari juu ya mradi huo ambao umefadhiliwa na Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa kwa kushirikiana na Shirika la viwango Tanzania (TBS).Picha na Vero Ignatus.
Muwakilishi wa Shirika la Mazingira Umoja wa Mataifa Clara Makenya akifafanua jambo kwa wanahabari kuhusu uhafifu wa bidhaa ,mazingira .Picha na Vero Ignatus.
Baadhi ya wadau wa waliohudhuria mkutano wa majadiliano kuhusu uboreshaji wa viwango wakifuatilia mazunguzo kwa makini.Picha na Vero Ignatus.
Wakwanza kushoto ni mkuu wa wilaya ya Ngorongoro Rashid Taka ,aliyepo katikati ni mkuu wa wilaya ya Arusha Gabriel Daqarro akifuatiwa na Mary Meela ambaye ni Meeja viwango (Tbs )na mratibu wa mradi huo.
Baadhi ya wadau wa mkutano wa majadiliano kuhusu uboreshaji wa utekelezaji wa matakwa ya viwango uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha kimataifa (AICC) wakiwa katika picha ya pamoja katika mkutano huo wa siku moja.
No comments