MWENYEKITI UVCCM ARUSHA APANDISHWA KIZIMBANI NA VERO IGNATUS ARUSHA


MWENYEKITI wa Umoja wa Vijana Mkoa wa Arusha (UVCCM), Lengai ole Sabaya (29)amefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha kwa makosa miwili ikiwemo kujifanya mtumishi wa umma idara ya usalama wa Taifa (TISS).
Sabaya alifikishwa mahakamani hapo 19 septemba  akitokea polisi kisha kuwekwa mahabusu kwa muda na kusomewa mashtaka hayo miwili.
Image result for uvccm arusha
Mwenyekiti wa Uvccm Arusha Lengai Ole Sabaya picha na Maktaba

Akimsomea mashtaka hayo mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Gwantwa Mwankuga, wakili wa serikali Lilian Mmassy alidai kuwa kosa la kwanza linalomkabili Sabaya ni la kujifanya mtumishi wa umma ambapo Mei 18 mwaka huu hoteli ya Sky way iliyopo makao mapya Jijini Arusha alijifanya kuwa mwajiriwa wa Usalama wa Taifa (TISS).

Kosa la pili katika siku isiyofahamika wala tarehe mwaka huu alighushi nyaraka za kitambulisho cha usalama wa Taifa chenye picha yake na kutumia namba Saturday. Code. Eagle 3 idara ya usalama wa Taifa chenye namba MT. 86117

Hata hivyo Sabaya alikana makosa hayo na ndipo wakili wa Serikali, Mmassy aliposema upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na dhamana ya mshtakiwa ipo wazi.
Hapo ndipo Wakili wa mshitakiwa, Yoyo Asubuhi alipomuomba Hakimu Mwankuga kumpa dhamana mteja wake kwakuwa ni haki yake ya msingi.

Naye Hakimu Mwankuga alisema kwakuwa dhamana ipo wazi anampa masharti  Sabaya ambayo ni kuwa na wadhamini wawili wakuaminika ikiwemo kusiani hati ya dhamana ya sh, milioni 3 kwa wadhamini wawili kila mmoja.

Hata hivyo wadhamini hao walikidhi masharti ya dhamana ya Sabaya na hatimaye kuachiwa kwa sharti la kufika mahakamani kila tarehe yake kesi na endapo atapata udhuru atoe taarifa mahakamani kupitia kwa wadhamini hao.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Oktoba 5 mwaka huu, alipotoka mahakamani Sabaya alizungumza na waandishi wa habari na kusema kuwa hiyo ni heshima ya kubwa kwake yeye kupelekwa mahakamani ambapo atapata nafasi ya kuwaumbua wanaopika majungu na fitina.

Amesema wapika majungu hao wamepata nafasi ya kucheza dakika 45za kutengeneza majungu dhidi yake na anaamini dakika 45zilizosalia zitachezwa ndani ya jengo tukufu la mahakama linalotenda haki.

Amesema wapo mchwa waliopo ndani ya chama wanaoshirikiana na upinzani na dunia nzima inawajua na mamlaka husika zimeshindwa kuwachukulia hatua na kuhoji kwanini mambo haya yabafanyika sasa ikiwa ni siku chache baada ya aliyekuwa Katibu wake, Ezekiel Mollel kufikishwa mahakama ya Mwanzo Maromboso na kusomewa shtaka la kufanya vurugu. 

Amesisitiza baada ya kutoka mahakamani hapo ataenda ofisi na kuita kamati ya utekelezaji pamoja na kamati ya uchumi na miradi ili kumpangia majukumu ya kazi, Said Goha ambaye ni Katibu wa sasa wa Umoja huo.

No comments