Vita vya kwanza vya ndege zisizo na rubani duniani, sura mpya katika mzozo wa India na Pakistan
Vita vya kwanza vya ndege zisizo na rubani duniani, sura mpya katika mzozo wa India na Pakistan

Chanzo cha picha,NurPhoto via Getty Images
Vita vya kwanza vya droni duniani vilizuka kati ya majirani wawili wenye silaha za nyuklia huko Asia Kusini.
Alhamisi iliyopita, India iliishutumu Pakistan kwa kurusha wimbi la ndege zisizo na rubani na makombora katika kambi tatu za kijeshi katika eneo la India na eneo linalodhibitiwa na India la Kashmir, mashtaka ambayo Islamabad ilikanusha haraka.
Pakistan, kwa upande wake, ilidai kuangusha ndege 25 za India, lakini Delhi imekaa kimya rasmi juu ya suala hilo. Wataalamu wanasema mashambulizi ya kulipiza kisasi yanaashiria mwanzo wa awamu mpya na hatari katika uhasama wa muda mrefu wa nchi hizo mbili, ambapo pande hizo mbili zinashambuliana kuvuka mpaka usio na utulivu sio tu kwa vifaru bali pia kupitia silaha zisizo na rubani.
Wakati Marekani na mataifa mengine yenye nguvu duniani yametoa wito wa kujizuia kwa pande zote mbili, eneo hilo liko kwenye ukingo wa mvutano usio na kifani, ambapo ndege zisizo na rubani - zinazohudumu kimya kimya na zisizoonekana - zimefungua ukurasa mpya katika mzozo wa India na Pakistan.
Nchi hizo mbili zilitangaza kusitisha mapigano lakini hivi karibuni zilishutumu kila mmoja kwa kukiuka
Chanzo BBC
No comments