Nchi 10 zenye nguvu kubwa zaidi za kijeshi Afrika 2025
Nchi 10 zenye nguvu kubwa zaidi za kijeshi Afrika 2025

Chanzo cha picha, Reuters
Uwezo huo wa kijeshi unashawishiwa na miungano, uhusiano wa kidiplomasia na hatua zilizopigwa katika teknolojia.
Hapa barani Afrika, Mataifa ya Misri, Algeria, na Nigeria ndio yaliyoorodheshwa katika mstari wa mbele kama yanayoongoza kwa uwezo wa kijeshi yakionesha uwekezaji mkubwa katika bajeti za ulinzi ili kuboresha miundombinu na kupata silaha za hali ya juu.
Mataifa yaliyostawi kiuchumi kama vile Misri na Afrika Kusini yametanguliza matumizi ya ulinzi katika bajeti zake ili kudumisha usalama, huku mataifa mengine yakikabiliwa na changamoto za migogoro ya ndani, vikosi vya kijeshi, na vikosi visivyo na ufadhili wa kutosha kukabiliana na waasi.
Licha ya uwezo wa kikanda, wanajeshi wa Afrika wamesalia nyuma ikilinganishwa na mataifa yaliyoendelea kwa sababu ya tofauti katika ugawaji wa bajeti, teknolojia, mafunzo na ufikiaji wa kimkakati.
Kulingana na Global Firepower, hizi hapa ni nchi 10 za Afrika zenye nguvu kubwa zaidi za kijeshi mwaka 2025.
No comments