Majina ya wafungwa 12 waliopewa msamaha na Rais Dkt Shein

Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Rais wa Zanzibar, Dkt Ali Mohamed Shein, ametoa msamaha kwa wafungwa 12 ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya sherehe za miaka 54 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Rais Dkt Shein ametoa msahama kwa wafungwa hao ambao walikuwa wamehukumiwa kwa makosa mbalimbali.

Msamaha huo umetolewa kwa mujibu wa ibara ya 59 ya Katiba ya Zanzibari ya mwaka 1984 ambayo imempa Rais mamlaka ya kutoa msamaha kwa wafungwa. 

Msamaha huo unatolewa kwa wafungwa kama nafasi ya wao kuanza kuishi maisha mapya na kuachana na vitendo vya kihalifu.

Wafungwa waliopewa msamaha huo ni;

   Abdul-Aziz Abdalla

    Omar Abdalla Nuhu

    Ali Khamis Mrau

    Mussa Ali Vuai

    Hassan Seif Khamis

    Nassor Abeid Issa

    Jihadi Jalala Jihadi

    Edward Jemeria Magaja

    Sleiman Abdalla Amir

    Mtumwa Khamis

    Said Seif Omar

    Masoud Seif Nassor


Katika hatua nyingine, raia wengi 74 wa Zanzibar (baadhi yao wamefariki) wametunukiwa medali na Rais Dkt Shein kutokana na mchango wao mkubwa katika mapinduzi na pia kuleta maendeleo katika visiwa hivyo.

Miongoni mwao, raia 43 wamepewe medali za mapinduzi huku wengine 31 wakipewa medali za mfano kwa utumishi wao uliotukuta kwa wananchi.



No comments