MIRADI VIPORO KUKAMILIKA KABLA YA MWEZI JUNI, 2016

Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Athumani 
Juma Kihamia amewaagiza watendaji wa Kata kukamilisha miradi yote viporo iliyopo kwenye Kata kabla yakuanza kutekeleza miradi mipya
iliyopitishwa katika kata husika.

Kihamia ameyasema hayo wakati akizungumza na watumishi wa Serikali katika Kata ya Muriet na Terati wakatiwa ziara ya kutembelea Kata zote 25 za Jiji la Arusha ambapo ziara hiyo imekamilika katika kata ya Muriet.

Amesema kuwa lengo hasa lakutembelea Kata zote na kuonana nawatumishi hao ni kuwakumbusha watumishi wajibu wao na kufanya kazikwa kuzingatia Miiko na Maadili ya Serikali huku na kuhakikisha kwamba shughuli zote za kwenye Kata zinafanyika kwa kuzingatia Sheria,kanuntaratibu na miongozo iliyopo

 "Siyo kwamba watumishi wangu wa Halmashauri hawafanyi kazi bali nikuwakumbusha majukumu yao katika kutumikia wananchi hasa katika kasi ya Serikali ya awamu ya tano ya hapa kazitu ambayo inatutaka tuwekaribu zaidi nawananchi wetu na mimi kama Mtendaji
Mkuu lazima nisimamie
kikamilifu“Alisema Mkurugenzi Kihamia.

Kupitia Kikao hicho amewataka watendaji wote Kuhakikisha kwamba Miradi viporo iliyopo kwenye Kata na Mitaa inakamilika kabla ya mwezi Juni ilikuweza kuleta Tija kwa wananchi nasikuanza kutekeleza miradi mipya nakuacha Fedha na nguvu zikipotea katika miradi ya miaka ya nyuma ambayo haikukamilika.

Alisema kuna miradi ya mwaka2015/2016 ambayo Fedha zimeshakutumika lakini haikukamilika sasa endapo tutaiacha tena mwaka huu miradi hiyo itaanza kuharibika na kukosa thamani kabisa hivyo tukapoteza Fedha za Serikali ambazo zilishaingizwa kwenye miradi hiyo ni vyema
tukaikamilisha ndipo tuanze miradi
mipya.

Vile vile alisema kuwa watendaji wa Serikali wanatakiwa wajitume kwa nguvuzote wasisubiri mpaka viongozi wa juu wafike kwenye maeneo yao na wananchiwalalamike wakati kuna kiongozi katika maeneo hayo ambao wanalipwa na Serikali ilikusaidia wananchi.

 " Hatutaki Mwananchi atoke kwenye Kata mpaka kwa Mkuu wa Mkoa au Mkuu wa Wilaya kwenda kulalamikia masuala madogo  madogo wakati kunakiongozi ambaye tumemuweka ili atatuekero akitokea Mtumishi wa hivyo ajue kwamba hatoshi kuongoza wananchi"Alisema Kihamia.

Ameongeza kuwa kwasasa anahakikisha Huduma zinaboreshwa katika Jiji la Arusha kwa kumjengea Mtumishi uwezo wa kufanya kazi bila kuogopa changamoto zilizopo nakuwa jasiri wakati anaongoza wananchi kwenye maeneo yao.

Hata hivyo amewagiza watumishi hao wa Serikali wakiwemo watendaji kutekeleza kwa muda uliowekwa mambo muhimu kama Utoaji wa Mikopo kwa vikundi vya vijana na Wanawake,kuainisha biashara zilizopo kwenye maeneo yao ya Utawala ikiwemo idadi ya mabango na maduka yotemajengo ,maeneo ya wazi pamoja na miradi viporo

No comments