POLISI NANE WAUAWA KWA KUPIGWA RISASI PWANI...RAIS MAGUFULI AWALILIA
Dar es Salaam.
Rais John Magufuli amepokea kwa mshtuko na masikitiko makubwa taarifa za vifo vya Askari Polisi wanane waliouawa kwa kushambuliwa na watu wenye silaha jana jioni katika eneo la Jaribu Mpakani, Wilaya ya Kibiti Mkoani Pwani.
Taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Ikulu leo inasema askari Polisi hao walikuwa wakitoka kubadilishana doria wameshambuliwa kwa kupigwa risasi wakiwa wanasafiri kwa gari katika barabara ya Dar es Salaam – Lindi.
No comments