Mitambo ya Bilioni 1.7 yazinduliwa Jijini Arusha

 Mitambo ya Bilioni 1.7 yazinduliwa Jijini Arusha 

Na. Vero Ignatus, Arusha

Hafla ya uzinduzi wa malori mapya na mtambo mpya wa kutengeneza miundombinu ya barabara  imefanyika Leo katika uwanja wa gymcana Jijini Arusha ambao inatahamani ya shilingi za Ki Tanzania Bilioni 1.7 ambapo itatumika kukarabati miundombinu katika barabara za pembezoni

Akizungumza katika uzinduzi huo mgeni rasmi  Meya wa Jiji la Arusha Macmillan Kirage amesema kuwa pesa ilitotumika kununua mirambo hii imetokana  na mapato ya ndani ya Jiji la Arusha ambapi amesisistiza kuwa  Mitambo hiyo itahusika na ukarabati wa barabara zinazohusiana na Jiji, ambazo haziko chini ya usimamizi wa TARURA.
Arusha

Mhe. Meya alisema Arusha ni Jiji la kitalii hivyo amewasihi viongozi kuwahamasisha wananchi kupanda miti kwani kila halmashauri imepewa kama vile walivyopewa jukumu la kuhakikisha linapanda miti Mil1 yote hayo ikiwa ni kuhakikisha kuwa Arusha inakuwa ya kijani. 

"Hamasisheni wananchi kuhakikisha mnatunza mazingira vile vile hakikisheni kuwa hawatupi chupa za plastiki pembezoni mwa barabara kwenye daladala, mabasi ya abiria ili wazingatie usafi na Jiji like safiAlisema
Arusha

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Jiji la Arusha   John Kayombo  amesema mitambo hiyo imekuja ikiwa ni hatua muhimu ya kumaliza changamoto ya barabara mbovu katika maeneo mengi ya jiji hilo 

 Kayombo, amesisitiza kuwa ununuzi wa mitambo hiyo ni matokeo ya juhudi za halmashauri kuhakikisha barabara za mitaa zinafanyiwa marekebisho kwa ufanisi, na kumaliza changamoto kubwa ya miundombinu ya barabara.

Akisoma ripoti fupi mbele ya ngeni rasmi ya ununuzi wa mitambo hiyo Mhandisi wa Jiji la Arusha Jacobo Mwakyambiki amesema mitambo hiyo inathamani ya bil. 1.7 Lego likiwa nikukarabati miundombinu Jiji la Arusha




No comments