Watu wenye ulemavu waliovuka changamoto na kufikia mafanikio


Watu wenye ulemavu waliovuka changamoto na kufikia mafanikio

w

Chanzo cha picha,Sophia Mbeyela

Maelezo ya picha,Sophia Mbeyela, Mwalimu na Mwanaharakati wa haki za walemavu Tanzania

Katika ulimwengu ambao mara nyingi huhusisha mafanikio na ukamilifu wa kimwili na kiakili, ni muhimu kufahamu kuwa kuna watu wenye ulemavu ambao wameweza kuvuka changamoto hiyo na kutenda mambo makubwa ambayo yanaweza kuwa mfano wa kuigwa duniani.

Katika historia, watu wengi maarufu wenye ulemavu sio tu kwamba wamebadili mtizamo na matarajio ya jamii kwamba hawana uwezo , lakini pia wameacha alama isiyofutika katika nyanja zao husika.

Katika Makala haya tunawaangazia baadhi ya watu wenye ulemavu ambao wamekuwa mashuhuri kwa kushinda changamoto ya ulemavu na kufikia mafanikio ya hali ya juu katika Nyanja zao. Hawa ni baadhi yao.

Sophia Mbeyela

f
Sophia Meyela ameweza kupata tuzo mbali mbali za kitaifa na kimataifa kutokana na kazi yake ikiwemo Tuzo ya Message of hope awards kutoka Marekani mwaka 2024

Sophia Mbeyela, ni mwanaharakati wa haki za walemavu nchini Tanzania mwenye ulemavu. Licha ya changamoto hiyo ameonekana kuwa mwanamke mwenye uwezo wa kuelimisha jamii, pia ameweza kujitoa kuwasaidia watoto wenye mahitaji maalumu walio katika makundi matatu -albino, walemavu wa viungo na yatima.

Sophia ambaye ni mwalimu wa sekondari ni Mkurugenzi mkuu na Muasisi wa taasisi ya walemavu -Peace Life for Persons with Disability Foundation (PLPDF) , shirika lisilo la kiserikali nchini Tanzania, linalowatetea na kuwawezesha watu wenye ulemavu ili kuwa na maisha huru na yenye kuridhisha.

Alilianzisha shirika hilo mwaka wa 2015 na kusajiliwa rasmi mwaka wa 2017, na tangu wakati huo limekuwa likitoa elimu ya ujasiriamali, msaada wa kiuchumi, na hatua za kujitambua ili kuimarisha ustawi wa watu wenye ulemavu kote nchini.

‘’ Wazo la kuanzisha NGO lilikuja kutokana na kwamba mimi mwenyewe nimo ndani ya hilo kundi, niliona kuna pengo, katika jamii, wazazi, na watu wengi kwa ujumla hawajapata elimu kuelewa kuwa mtu mwenye ulemavu wana uwezo. Nilitaka kuonyesha kuwa hata kama mimi ni mlemavu nina uwezo wa kufanya zaidi ya vile wanavyofikiria’’, Sophia aliieleza BBC. 

Mafanikio

w

Chanzo cha picha,Sophia Mayela

Kupitia taasisi yake (PLPDF) Bi Sofia mejitolea binafsi kuwa mfano wa kuionyesha jamii ya watu wenye ulemavu kuwa wanaweza kuishi maisha mema iwapo wataweka bidii katika uwezo walio nao.

‘’Nimeweza kutoa elimu kubwa na kuhakikisha ujumuishi wa watu walemavu katika shughuli za kijamii’’, anajivujia Bi Mbeyela.

Mipango ya kielemu ya shirika lake imeweza kuathiri maisha ya maelfu ya watu wenye ulemavu kwa njia chanya, kwa kuwapatia maarifa, ujuzi na fursa za maisha bora ya baadaye.

‘’Nimeweza kuonyesha kuwa watu wenye ulemavu wanaweza kutumia kitu chochote walicho nacho kufanya mambo ambayo yanaweza kuleta mabadiliko kwao na kwa jamii nyingine’’, anasema.

Kupitia shirika lake, ameweza kuchangisha pesa za ujenzi miundo mbinu inayowasaidia wanafunzi wanaoishi na ulemavu kusoma kwa urahisi ikiwemo shule ya sekondari ya wasichana jijini Dar es Salaam.

Kutokana na kazi zake ameweza kutambuliwa na kupata tuzo mbali mbali kama vile, Tuzo ya teknolojia ya mawasiliano kutoka Chuo cha ICT technology nchini Misri -2019, Tuzo ya mwanamke wa shoka kutoka radio ya EFM Tz, kipengele cha harakati za usawa - 2023 Kutoka Taasisi ya tisha mama TZ - kwa harakati za elimu -2023. Panafrican awards - humanity and social justice awards- 2017, Tuzo ya Malkia wa nguvu awards Tz -2017 , 6 Tuzo ya Mwanamke hodari -2023 kutoa global peace foundation Tz na Tuzo ya Message of hope awards kutoka USA -2024.

Kwa sasa anapambana kuhakikisha kuwa vifaa vinavyotumika kama viungo mbadala kwa watu wenye ulemavu ambavyo ni bei ghali vinapatikana kwa bei rahisi nchini Tanzania, na kuweza kuwafikia walemavu kuanzia mashinani Tanzania.

Chanzo BBC. 







.

No comments