Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kongwa afariki dunia baada ya gari lake kuangukiwa na lori la mafuta


Mkurugenzi wa Manispaa ya Kongwa, Izengo Ngusa, amefariki asubuhi ya leo Aprili 15 kwenye ajali ya gari,
Taarifa zilizotufikia zinasema gari dogo alilopanda Mkurugenzi huyo, lenye namba za usajili T619 DMA aina ya Toyota Crown Athlete, liliangukiwa na lori lililobeba mafuta,
Ajali hiyo imetokea eneo la Mbande Makaravati mkoani Dodoma.

Lori la mafuta lililoiangukia gari ya DED wa Kongwa, Mhandisi Ngusa Izengo limefanikiwa kuondolewa. 

Lakini mwili wa Izengo umeshindwa kunasuliwa kwenye gari yake kutokana na kuungana na kugandia kwenye vyuma. 

Gari hiyo imepelekwa mjini Dodoma ambapo utaalamu zaidi utatumika kuinasua maiti iliyopo.!

No comments