JESHI LA POLISI LINAMSHIKILIA MAMA ANAYE TUHUMIWA MUUA MTOTO WAKE KIKATILI, WATU WENGINE

 JESHI LA POLISI LINAMSHIKILIA MAMA ANAYE TUHUMIWA MUUA MTOTO WAKE KIKATILI, WATU WENGINE WAJERUHIWA


Dar es Salaam — Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linamshikilia Zuhura Juma maarufu kama Matengo kwa tuhuma za kumuua kwa ukatili mtoto wake wa miezi saba, Shufaa Abdallah, na kujeruhi watu wengine wawili.

Kwa mujibu wa taarifa ya Polisi, tukio hilo la kusikitisha lilitokea mnamo Juni 30, 2025, saa sita mchana katika maeneo ya Nyumbanyeupe, Majimatitu, Wilaya ya Temeke. Inadaiwa kuwa mtuhumiwa alitumia kitu chenye ncha kali kutekeleza unyama huo.

Watu wengine wawili walioumia katika tukio hilo wametambulika kwa majina ya Agnes Mathias na Suleiman Abdallah, ambao kwa sasa wanaendelea kupatiwa matibabu.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam amesema kuwa uchunguzi wa awali unaendelea kwa kushirikiana na taasisi nyingine za kisayansi ili kubaini chanzo cha tukio hilo. Mara uchunguzi utakapokamilika, hatua nyingine za kisheria zitafuata.

Tukio hili limezua masikitiko na taharuki kwa wakazi wa eneo hilo, huku jamii ikihimizwa kushirikiana na vyombo vya dola kutoa taarifa zozote zitakazosaidia kukamilisha uchunguzi.

No comments