MAONYESHO YA 4 YA Utalii yafanyika mkoani Kilimanjari



Na Vero Iganatus ,Kilimanjaro




Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira alizungumza katika maonyesho hayo yaliyofanyika chuo cha ushirika Moshi.
Mkurugenzi wa Kilifair Dominick Shoo akaizungumza katika ufunguzi wa maonyesho ya nne ya kulifair

Waziri wa maliasili na Utalii Hamis Kigwangala akizungunza wakati wa uzinduzi maonyesho ya utalii.
Na Vero Iganatus ,Kilimanjaro

Maonyesho ya Kimataifa ya Utalii ya (KaribuKilifair )yamezinduliwa rasmi leo na Waziri a Utali na maliasili Hamisi Kigwangala katika uwanja wa chuo cha ushirika wilayani Moshi mkoani Kilimanjaro yakiwa ni ya nne ambapo zaidi ya makampuni 4000 kutoka duniani yameweza kushiriki.

 Kigwangala amewapongeza Karibufair pamoja na Kilifair kwa kuunganisha matamasha  hayo mawili ya kutangaza vivutio vya utalii nchini amabapo amesema hakuna ushindani wa ndani bali na ushirikiano bali upo ushindani wa nje.

Amesema mpango  wa Taifa wa maendeleo wa miaka 5 unaelekeza mambo kadhaa kwenye sekta ya utalii,ikiwemo kuboresa mazingira ya kufanya biashara,leseni ya wakala wautalii amabapo serikali imerahisisha kutengeneza dirisha moja la kuoza tozo mbalimbali,dirisha la kodi,kurahisisha usajili wa biashara pia utoaji wa vibali mbalimbali

Katika jitihada hizo amesema mambo kadhaa yamefanyika likiwemo ya uzitazama baadhi ya tozo na kuziondoa ,kama ile ya TALA leseni ya wakala wa utalii,amabapo serikali imeshusha tozo sawa na shilingi za kitanzania sawa na dola 200 hadi dola 500

’Dola hizi 500 ni kwa kampuni amabayo itkuwa na magari kati ya  1hadi3,kwa hiyo ukiwa na gari moja safari hii unaweza kuingia tofauti na zamani ilikuwa lazima uwe na magari matano”alisema Kigwangala.

Kwa upande wake mkurugenzi wa Kilifair bwana Dominick Shoo amesema kutokana na mjumuiko wa maonyesho hayo watahakikisha kuwa kila mkoa shiriki unapata stahiki yake ya kifedha nakisapot kutoka katika maonyesho hayo 

Shoo ametoa sababu kwanini kiingilio ni shilingi 8000 ,amesema dhumuni kubwa haswa  wanahitaji watu ambao wanaweza kufanya biashara katika maonyesho hayowakiwa na lengo maonyesho yasiwe na watu wengi amabao hawana sababu za msingi bali aweze kupata fursa ya kujifunza biashara

Aidha amesema katika makubaliano yao waliamua kwamba kipindi kijacho  maonyesho hayo yatafanyika mkoani Arusha

No comments