Mahakama Kanda ya Arusha yasimamisha Amri iliyotolewa na serikali ya kuwataka kufuta kata Vijiji vitongoji Ngorongoro

Mahakama Kanda ya Arusha yasimamisha Amri iliyotolewa na serikali ya kuwataka kufuta kata Vijiji vitongoji Ngorongoro

Na. Vero Ignatus, Arusha

Mahakama kuu kanda ya Arusha imesimamisha utekelezaji wa Amri iliyokuwa imetolewa na serikali kupitia tangazo LA serikali namba 673 ya mwaka 2024 la kufuta vijiji na kata na vitongoji katika wilaya ya Ngorongoro 

 Uamuzi huo umetolewa na Jaji Ayubu Mwenda Augusti 22,2024 ambapo alisikiliza maombi madogo ya zuio yaliyowasilishwa na ndugu Isaya Ole posi mwananchi wa ngorongoro kwa kupitia Wakili wake Peter Njau 

Baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili, Jaji Mwenda aliridhia maombi hayo madogo na kukubali zuio la kusimamisha tamko hilo kupisha usikilizaji wa maombi ya msingi ,hadi amri ya Mahakama itakavyoelekeza na vinginevyo.
Kwa upande wake Wakili wa kujitegemea Peter Njau alisema awaki kwa wananchi wa ngorongoro kuliweza kitokea taharuki kutokana na tangazo lililokuwa  umetolewa na serikali kupitia mamlaka ya mji mdogo wa ngorongoro la  kuwataka wakazi wake kuhama, Ila baada kusikikizwa kwa pande zote mbili Jaji aliweza outta Amri ya kuzuia

"Mteja wangu aliweza kuniomba kumuwakilisha katika shauri  kuweza kuomba Mahakama itazame uhalali wa Amri ole ni kuweza kuleta shauri lile mahakamani na kulisajili maombi madogo na yalisikilizwa kwa pande zote mbili na aliweza kudos Amri ya kuzuia" Alisema Wakili Peter Njau"


No comments