KUKITHIRI KWA MIGOGORO YA ARDHI YATAJWA KUWA CHANZO KIMOJAWAPO CHA MAUAJI -ARUSHA
![]() |
| Baadhi ya Majaji wakiwa katika maadhimisho ya wiki ya sheria yakiyofanyika katika Mahakama kuu kanda ya Arusha |
![]() |
| Mkuu wa mkoa wa Arusha John Mongela maadhimisho ya wiki ya sheria yaliyofanyika katika Mahakama kuu kanda ya Arusha |
KUKITHIRI KWA MIGOGORO YA ARDHI YATAJWA KUWA CHANZO KIMOJAWAPO CHA MAUAJI -ARUSHA
Na.Vero Ignatus,Arusha
Majaji na Mahakimu wametakiwa kuwa na utu katika mashauri mbalimbali wanayosikiliza na kuyatolea maamuzi, pamoja na kupinga vitendo vya rushwa ambayo ni adui wa haki,ambapo wiki hiyo imekwenda sambamba na mwaka wa kazi Kimahakama wa mwaka 2022
Hayo yamesemwa na Jaji Mfawidhi kanda ya Arusha Mosses Mzuna ,Katika kuadhimisha kilele cha wiki ya sheria 2/2/2022,ambapo aliekemea mambo yanayotokea mkoani humo ikiwemo kukithiri kwa mauaji kwa wanafamilia au jamii, ambayo baadhi hutokana na migogoro ya ardhi,ubomoaji wa majengo/ nyumba bila amri halali, wakati kuna mashauri yanaendelea mahakani,pamoja na kutumia madalali ambao hawajasajiliwa.
Mzuna alisema kumekuwa na kitendo cha kuchelewa kwa upelelezi wa
mashauri na kuchukua muda mrefu, jambo
ambalo husababisha kudhoofisha kasi ya
usikilizwaji wa mashauri kwa wakati,Ambapo amesema tatizo hilo lisipotibika hawataweza kutimiza malengo
ya kumaliza mashaurikwa wakati,hivyo amezitaka ofisi zinazohusika lisimamie
jambo hilo
Aidha amesema changamoto ambayo wanakabiliana nayo ni pamoja na wanafamilia kutokufungua mashauri ya mirathi mahakamani kwa wakati, hivyo kuchochea migogoro ya kifamilia na hatimaye kupelekea mashauri ya msingi kuchelewa,pia jamii kutokutumia njia ya usuluhishi kama njia mbadala hadi h,upekelea kufikishana mahakamani hata kama suala ni dogo
‘’Ardhi
isiwe sababu ya kusababisha hadi sisi wana arusha kuuwana jamani ,halafu
mnasubiria siku ya mahakama ndipo mnakwenda kuvunja kweli?msiwasababishe majaji
na mahakimu waonekane hawana maamuzi sahihi, Harutakubali majaji na mahakimu
simameni katika haki wasiwepo watu kukuonyesha wewe kesi ipo mahakamani lakini
anakuja kuvunja simameni kidete katika hili’’Alisisitiza Jaji Mzuna
![]()
Kwa upande wake mkuu wa
mkoa John Mongela ameupongeza uongozi wa mahakama ya Arusha kwa kazi
kubwa inayofanyika katika wiki nzima iliyopita, kwa kujihusisha na jamii kwa
kutoa msaada wa kisheria ,kwani kulikuwa na baadhi ya mambo yalikuwa katika ofisi yake
ambapo baadhi wananchi wametoa shuhuda, kwamba wamefahamu jambo gani wafanye
ili kupata haki zao.
Mongella alisema
kuwa jambo hilo limenawasaidia mihimili
mingine katika kuhakikisha kunakuwa na utulivu kwa jamii,kwani kazi kubwa
inayofanywna mahakama inachangia kwenye majukumu yao ya kiutendaji,pamoja na
kuhakikisha usalama na utulivu kuwepo ,hivyo ameahidi kuwa
karibu na mahakama pale wanapohitajika na kuhakikisha kwamba mhimili huo
unakuwa imara zaidi.
Kwa upande wake wakili wa serikali mfawidhi aliyeiwakilisha ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali Veritas Mlay alisema katika kuelekea mahakama ya mtandao katika zama za mapinduzi ya nne ya viwanda inaondoa mipaka kati ya utaratibu ulikuwa umezoeleka kwa muda mrefu wa mtu kuzoeleka kuwepo mahali Fulani kimwili na kutumia utaratibu wa kidigitali wa matumizi ya tehama
Amesema kwa upande wa mahakama 2015-2016 iliweka azma Madhubuti ya kuweka marekebisho makubwa katika mfumo wa matumizi ya tehama kwa ujumla,aidha hatua ya maboresho kuelekea mahakama ya mtandao ilikolea Zaidi mwaka 2018 ambapo Jajimkuu wa Tanzania alitoa kanuni ya ufunguaji mashauri kwa njia ya mtandao kupitia tangazo la serikali no 148 ambazo zimewezesha mashuri kufunguliwa masaa 24.
Amesema mabadilio ya maisha na ufanyaji biashara na mambo mengine yanayotokea katika Maisha ya mwanadamu kipekee yanakwenda sambamba na huduma ya utoaji haki,hivyo huduma za utoaji haki hazina budi kuendeshwa kwa njia ya kimtandao
Amesema mapinduzi hayo yan ne yameongeza ufanisi kuanzia pale matumizi ya kwanza hadi ya tatu yalipofikia ambapo mapinduzi ya kwanza yalitokea katika karne ya 18 ambapo binadamu aligundua mashine ya kuwezesha uzalishaji kwa mara ya kwanza duniani,ya pili yalileta ugunduzi wa mafuta ya nishati na umeme pamoja na maendeleo mengine ya kisayansi,mapinduzi ya tatu yalianza 1950 ambapo vya tehama kama tarakishi viligundulika
Kwa upande wake mwenyekiti wa mawakili wa kujitegemea George Njooka alisema kuwa tasnia ya sheria iangalie kwa kina juu ya bongo bandia (Artificial Teligency) ielekezwe kwenye kuelewa ubongo wa binadamu na kuchakata matumizi yakuwa sahihi na bora ya tehama ili kubresha utoaji haki kwa wananchi na kutatua changamoto zinazoikabili jamii
Alisema kuwa kukua kwa bongo bandia kunaweza kuleta maendeleo kwa utoaji wa haki nchini hivyo sekta hiyo haina budi kujizatiti na kujiandaa kufanya maandalizi mwananaili muda ukifika maboresho ya utoaji haki na ushauri ya kisheria uelekezwe kwenye usahihi wa taarifa na sheria husika ili haki ya mwananchi ionekane kufanyika kwa muda mfupi
Alihitimisha kwa kusema kuwa ili waweze kwenda kwa kasi katika kuleta maboresho kuelekea mahakama mtandao inahitajika kuhakikisha kuwa jamii inakubaliana na hayo ya kutegemea bongo bandia na matumizi ya tehama katika utoaji haki sambamba na elimu ya kutosha itolewe ili mapokezi yake yawe chanya .
Mwisho



No comments