TANZANIA YAPIGA HATUA KATIKA SEKTA YA BARABARA


Na. Vero Ignatus, Arusha

Serikali ya Tanzania  imefanikiwa  kuboresha   ujenzi  wa  barabara  kwa kutumia Teknolojia ya kuchanganya  lami  Kulingana  na  Mazingira  husika  katika  kanda  mbalimbali  Nchini na ipo teyari kwa ajili ya uwekezaji kwa maendeleo ya uchumi wa taifa . 

Akizungumza na waandishi  wa habari  mkoani  Arusha Waziri  wa ujenzi uchukuzi na mawasiliano Mhandisi Isack Kamwele katika  mkutano wa  kimataifa  Mhandisi  amesema  wakala  wa  barabara  nchini   Tanroads   wameanzisha  miongozo  ya  kuchanganya  lami  Kulingana  na Mazingira  ya     hali  ya hewa  ya  mikoa  mbalimbali  ili  kuweza  kujenga  barabara  imara zitakazoendana  na  mazingira husika. 

Ameleza kuwa Tanzania  kutokana  na  mikutano hiyo wameweza kufanikiwa kutengeneza  Teknolojia  mpya ya kuchanganya  lami  kutokana na mazingira na jiografia ya maeneo  ambapo mfano  lami inayojengwa  Katavi  itaendana  na  hali  ya  hewa  ya Mazingira  yake  ili  barabara  zisiharibike na kudumu kwa muda mrefu hivyo kusaidia kukuza uchumi. 

Amewata  wataalamu  wa  TANROADS kutofanya  kazi  Kwa  mazoea  na  pia  kuhakikisha  wanatatua matatizo  ya  sehemu  zao  za  kazi wasisubiri hadi  mamlaka  za  juu  kuwapangia  majukumu  yanayowahusu. 
Kwa upande wake Mkurugenzi wa TPA Deusdedit Kakoko akiongea kama mshiriki wa mkutano huo amesema kuwa mkutano huo umekuwa ni sehemu muhimu kwao kama mamlaka ya bandari wamejipanga kutumia mkutano huo kuboresha utendaji wao wa kazi

Kuangalia mabadiliko ya teknolojia ya usafirishaji na matumizi ya Tehama yatasaidia kuboresha na kubadilika kwa kwenda kwenye kizazi cha nne cha mapinduzi ya usafirisha duniani ambapo jambo hilo litaharakisha utoaji wa bidhaa katika bandari .

Kauli  mbiu  ya  mkutano  huo  ni  'Mapinduzi  ya  nne  ya  sekta  ya  usafirishaji  yanayohusiana  na mabadiliko  ya  kiuchumi  katika  nchi  zinazoendelea.

Mwisho.

No comments